Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika kufanya kwa vitendo kampeni ya usafi ya kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Sophia  Mjema akiwa kaongozana na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Mhe. Edward Mpogolo alitembelea kituo cha daladala cha stesheni na kukuta magari mengi ya abiria hayana vikapu vya taka, ambapo wameyatoza takribani magari saba  kiasi cha shilingi 50,000 kwa kila moja katika eneo hilo.
Huku kwa upande wa madereva wa bajaji wanaopaki eneo la Soko la Samaki Feri wamepewa onyo na kuombwa kufanya hivyo mara moja kabla hawajachuliwa hatua na mamlaka husika ya Halmashauri hiyo ya Ilala.
Katika hatua nyingine DC Mjema amewataka wafanyabishara wadogo wanaopanga bidhaa zao kandokando ya barabara iliyopo jirani na soko la samaki la Feri kujiandikisha kwa afisa mtendaji na kuondoka eneo hilo mara moja, huku akisema Halmashauri hiyo itawapangia maeneo ya biashara ndani ya soko hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...