Na Ali Issa, Maelezo Zanzibar.

Wizara ya Afya Zanzibar kupitia kitengo cha maradhi ya yasio pewa kipaumbele (kichocho, matende, na Vikope)kimo katika harakati za kuyatokomeza kabisa maradhi hayo katika maeneo ya Zanzibar.

Hayo yamesemwa leo huko Mkoa wa Kusini Unguja katika Hoteli ya visital inn Jambian na Dr.wa maradhi hayo Khalifan Abdalla Mohamed wakati wa semina ya mapitio wa mradi uliomaliza wa kuyatokomeza maradhi hayo .

Amesema maradhi ya kichocho na matende yaliathiri sana wananchi wa visiwa vya zanzbar katika miaka ya thamanini na kupelekea wengine kupata maradhi ya matende hadi hii leo jambo ambalo kwasasa maradhi hayo yanaonekana kutoweka kutokana na jitihada za Serikali na washirika wake wa maendeleo kulivalia njuga tatizo hilo.

Amsema kwa sasa hali hiyo inaridhisha kwakiasikikubwa na sehemuzilizo bakia nichache kuliitokomeza tatizohilo “Tuna tarajia kuyamaliza maradhi ya kichocgo na matende kwani imekuwa nadra kupokea wagonjwa wamaradhi haya ispokuwa niwale wale wagonjwa wazamani tu walioathirika na matende,kichocho,na  zipo baadhi ya maeneo ambayo hayajamalizika maradhi hayo kama vile kamgamba,kinyasini,moga,kizimkazi na kwapemba micheweni kwa”alisema DR Khalifan.

Nae mwenyekiti wa mradi wa kutokomeza maradhi hayo kutoka Nchini giniva katika shirika Global Schistosomiasis Alliance Dr Lorenzo Savioli amesema mapitio ya semina hiyo ni kuangalia vipi kuisaidia Zanzibar  kwa kuwapatia madawa na kufikia lengo la kuyatokomeza maradhi hayo.
Amsema  wananchi wazitumie dawa hizo kwa rika zote na hazina matatizo yoyote bali zinapoza zaidi maradhi mengine kama vile mapele mabaka na mipasuko mwilini.

Alisema wazitumie dawa hizo bure na nifrusa kwao ,kwani nchini kwao dawa hizo ni ghali mno kwa mwananchi wa Tanzania.

Nae mkurugenzi wa Maendeleo ya maji Zanzibar Muhamed Iliasa Mohamed alisema katika kuondoa tatizo la kichocho Zanzibar ni kuhakikisha kupeleka maji safi na salama katika maeneo yote ya zanzbar ili wananchi waweze kutumia maji safi na kuacha kutumia maji ya mito na mashimo.
Aidha alisema wanalazimika maji kuyatia dawa yakuulia vimelea vya maradhi hayo ili visiwe na nafasi ya kuathiri wananchi wanapo yatumia.
 Washiriki mbali mbali wa Semina wakifanya mapitio ya Mradi wa kutokomeza Maradhi yasiopewa kipaumbele (Kichocho,Matende na Vikope) katika ukumbi wa Hoteli ya VISITAL INN iliopo Jambiani Mkoa wa kusini Unguija.
 Mwenyekiti wa kutokomeza Maradhi hayo kutoka  Shirika la Global Schistosomiasis Alliance (GSA) Dr Lorenzo Savioli,akizungumza na waandishi wa Habari namna walivyodhamiria kuyatokomeza maradhi haya katika Nchi ya Zanzibar.
Mkurugenzi Maendeleo ya Maji Moh’d Iliasa Moh’d akizungumza na Waandishi wa Habari,  namna walivyokusudia kuwapelekea Wananchi huduma ya Maji maeneo yote ambayo yamegundulika na maradhi ya kichocho hayana maji salama watafikisha huduma ya Maji safi na salama haraka iwezekanavyo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...