Kiongozi wa bendi maarufu Ngoma Africa aka FFU-Ughaibuni yenye makao nchini ujerumani mwanamuziki Ebrahim Makunja almaarufu Kamanda Ras Makunja mapema tu alihojiwa na radio BBC Kiswahili katika kituo chao Mikocheni jijini Dar.
Akiongoza mahojiano hayo mtangazaji Omari Mkambala
alimlima maswali Ras Makunja ambapo katika moja ya majibu yake mwanamuziki huyo alisisitiza na kutoa wito kwa Watanzania walio nje ya nchi kuwa mstari wa mbele kwa kuwapa ushirikiano bendi na wanamuziki wa Tanzania pale wanapoziona fursa za kimataifa ili muziki wa Tanzania ufike nje ya mipaka na kupata soko zaidi la kimataifa
Kamanda Ras Makunja alisema muziki wa dansi na mengineyo ya Kitanzania ina nafasi nzuri nje ya nchi kama Watanzania wenyewe walio nje wakatakuwa na uzalendo wa kuzipigania  bendi za nyumbani kutumbuiza katika majukwaa kimataifa. msikose kusikiliza mahojiano hayo katika radio BBC idhaa ya Kiswahili.
 mahojiano hayo yaliongozwa na mtangazaji Omari Mkambala

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...