Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, amewataka wananchi wote kushirikiana na kusherehekea  miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara kwa kuunga juhudi za serikali ya awamu ya Tano ya kupinga ufisadi na rushwa nchini.
“Kwa niaba ya serikali natoa wito kwa wananchi wote nchini kusherehekea siku hii kwa kuwakumbuka waasisi wetu waliotetea na kutuletea Uhuru wa nchi yetu. 
"Aidha niwaombe wananchi wote kuunga mkono juhudi za Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika kuimarisha uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu” amesema Mhe. Mhagama.
Kauli mbiu ya sherehe za kutimiza Miaka 55 ya uhuru ni “Tuunge Mkono Jitihada za Kupinga Rushwa na Ufisadi na Tuimarishe Uchumi wa Viwanda kwa maendeleo yetu”
Mgeni Rasmi katika Maadhimisho hayo atakuwa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe.Jenista Mhagama akimsikiliza  Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Jackson Lyaniva wakati akikagua maandalizi ya maandhimisho ya miaka 55 ya Uhuru Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 8 Desemba, 2016 (katikati) ni Mkurugenzi wa Idara ya Maadhimisho na Sherehe za kitaifa Ofisi ya Waziri Mkuu Bi.Flora Mazelengwa  
Mtumishi katika wa Idara ya Maadhimisho na Sherehe za kitaifa Ofisi ya Waziri Mkuu  Bw. Hamad Hashim akisafisha  zuria wakati wa  maandalizi ya maandhimisho ya miaka 55 ya Uhuru Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam leo tarehe 8 Desemba, 2016.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Nafurahi kuona jamaa hajapiga stop sikukuu hii kama mwaka jana.

    ReplyDelete
  2. Hii ndiyoitkuwa sherehe ya kwanza ya kitaifa kwa JPM kuwa mgeni rasmi. Rais wetu ameonesha kwamba mambo yakianza kwenda mswano mambo kama haya yana umuhimu wake. Sio wakati ule shida kibao kila kona halafu mnatumia mabilioni ya shilingi kwa khanga na Tshirt. Hongera Rais wetu kipenzi cha wanyonge

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...