Na Mwamvua Mwinyi, Rufiji
TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) inawahoji watu 11 akiwemo Mtendaji wa kata, kijiji pamoja na vijana Tisa ambao ni wabeba mizigo (makuli) kwa madai ya kuchepusha chakula cha waathirika wa mafuriko Wilayani Rufiji kwa utaratibu usio rasmi.

Mkuu wa wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowelle alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusikitika endapo watu hao watabainika kufanya kitendo hicho.

Alielezea,yupo Mtendaji mmoja wa kata na Mtendaji wa kijiji ambao wakibainika watachukuliwa hatua za kiutumishi.


"Ni taarifa za awali ila kwa haraka haraka kuna mifuko zaidi ya 20 ilidaiwa kufichwa, tulivyobaini tuliaagiza wahusika warejeshe vyakula walivyoficha kisha kuwaripoti katika vyombo vya kisheria ,moja wapo kuhojiwa na TAKUKURU na baada ya uchunguzi watatoa taarifa ya kina."

Gowelle alieleza ,wanatumia vijana mbalimbali kubeba mizigo inayofikishwa kama misaada Rufiji na wanalipwa fedha , Kwahiyo ikitokea vitendo vya aina hiyo ni kuondoa uaminifu.

Aliwatahadhalisha vijana hao makuli kufanya kazi yao kwa uaminifu badala ya kuweka tamaa.

"Wasigeuze kufa kufaana, wafanye kazi yao ya kubeba vifaa, Vyakula Kwa uaminifu badala ya kuficha ama kujichukulia kinyume na taratibu na waache kuanzia sasa watafuatiliwa wakigundulika watachukuliwa hatua kali " alieleza Gowelle.

Pamoja na hayo alieleza ,Rufiji ni miongoni mwa wilaya iliyoathirika na changamoto ya mafuriko,Kati ya wilaya zilizopo kwenye mikoa 14 iliyokumbwa na changamoto hiyo.

Gowelle aliwaasaa, ambao bado wapo kwenye maeneo ya bondeni na yasiyo salama wahame ili kuondokana na changamoto zisizo za lazima.

Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi akizungumza wakati wa Mkutano wa Uchaguzi wa Viongozi wa Kati ya Uongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika leo tarehe 24 April 2024 Zanzibar katika ukumbi wa Spring Hall, uliopo Madinat Al Bahr Hotel.
Mjumbe wa Bodi ya Udhamini ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye alimwakiisha Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Ndg, Vuai Ali Vuai akitoa historia ya Baraza la Vyama vya Siasa wakati wa Mkutano wa Uchaguzi wa Viongozi wa Kati ya Uongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika leo tarehe 24 April 2024 Zanzibar katika ukumbi wa Spring Hall, uliopo Madinat Al Bahr Hotel
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Ndg. Juma Ali Khatibu akizungumza wakati wa Mkutano wa Uchaguzi wa Viongozi wa Kati ya Uongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika leo tarehe 24 April 2024 Zanzibar katika ukumbi wa Spring Hall, uliopo Madinat Al Bahr Hotel.
Mjumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara, Ndg. Salum Mwalim akitoa salam kwa niaba ya uongozi wa Baraza hilo wanaomaliza muda wao wakati wa mkutano wa uchaguzi wa viongozi wapya wa Baraza hilo uliofanyika leo tarehe 24 April 2024 Zanzibar katika ukumbi wa Spring Hall, uliopo Madinat Al Bahr Hotel. Kushoto ni Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi

Na: Frank Shija, ORPP
BARAZA la Vyama vya Siasa limeafiki kutoa pongezi za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kuimarisha Demokrasia nchini kwa kuboresha Baraza la Vyama vya Siasa nchini.

Hayo yamebainishwa na Makamu mwenyekiti wa Kamati ya Fedha ya Kamati ya Uongozi ya Baraza la Vyama vya Siasa ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Ndg. Salum Mwalimu wakati akitoa salaam kwa niaba ya Baraza hilo kabla ya uchaguzi wa viongozi wapya wa Kamati ya Uongozi ya baraza hilo uliofanyika tarehe 24 April 2024 Zanzibar katika Ukumbi wa Spring Hall Madinat Al Bahr Hotel.

“ Kuna wakati tumemuweka Jaji Mutungi kwenye kitimoto lakini ni wahakikishie tuendelee kuweka imani kwenye kamati ya uongozi, mtakumbuka hatukuwa na Bajeti kwenye Baraza la Vyama vya Siasa lakini chini ya kamati yenu tumefanyakazi kubwa sana mpaka leo msije mkasema na mpigia mtu kampeni lakini ndani ya miaka miwili tuna bajeti yetu iliyopitishwa Bungeni,na tumeandaa mikutano miwili mikubwa ambayo imeleta tija kubwa kwa Taifa letu, yote haya ni nia njema ya Serikali kuhakikisha Demokrasia inazidi kuimarika” Alisema Salum Mwalimu.

Aliongeza kuwa kuundwa kwa Kikosi kazi ni zao la Baraza la Vyama vya Siasa kilichotokana na Baraza hili kupitia Kamati ya Uongozi na Sekretarieti chini ya Jaji Francis Mutungi na tumefanikiwa kuandaa mikutano miwili ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa Bara na Visiwani.

“Mheshimiwa Jaji amesema kabla ya kikao cha Baraza kutakuwa na vikao vya Kamati jambo ambalo tumelipigania muda mrefu sana hii inaonyesha Dhahiri nia njema ya Serikali kuhakikisha Demokrasia inaimarika, mtaona kwa mara ya kwanza juzi kuna kadude kameingia kwenye vyama vyetu kuhakikisha tunasafisha karoti na kuhakikisha akaunti ipo active, kazi ile imefanywa kwa wivu mkubwa na kamati ya uongozi na kupokelewa na Jaji Mutungi na Sekretairieti na wakaitekeleza ndani ya muda mfupi, na mheshimiwa Jaji kuna jambo alilisema ambalo kilikuwa kilio chetu cha muda mrefu cha kamati kukakaa kabla ya Baraza” aliongeza Mwalimu.

Kwa upande wake Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi alisema kuwa wakati wanapanga mikutano ya Baraza la Vyama vya Siasa vitatanguliwa na vikao vya Kamati za Baraza la Vyama vya Sias ambavyo vipo kikanuni kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa.

“Ebu tulionyeshe Taifa ili kuwa tuliopo hapa tuna haki yakukutana na kujadiliana, jana nilitakakusema kwamba Kamati ya uongozi haiwezi kukaa kabla Kamati hazijakaa, kiutaratibu zinatakiwa zile kamati kukaa arafu wenyeviti wanakuja kutuambia yaliyojiri kutoka katika kamati zao” Ailisema Jaji Mutungi.

Jaji Mutungi aliongeza kuwa lengo la kuwa na vikao vya kamati kabla ya kikao cha Baraza ni kuhakikisha kuwa masuala yote yanayojadiliwa katika Baraza yawe yametoka chini kwenyevyama husika ikiwa ni njia sahihi ya kujenga na kuhimarisha Demokrasia na umoja wa kitaifa.

“ Sasa tunatakiwa tuboreshe taarifa zetu ambazo hwa wawakilishi wanaokuja kwenye Baraza zinakuwa zimeanzia chini kutoka kwenye vyama vyetu zilitwe kwenye kamati ya uongozi mwisho kwenye baraza ata mtu akisema Msajili mwenyewe ni Jaji mimi mwenye nakuwa na vitu ambavyo vimetokana na mfumo mzima ambao tumetokanao kwenye Baraza la vyama vya Siasa”. Aliongeza Jaji Mutungi.

Akizungumzia chimbuko la Baraza la Vyama vya Siasa Mjumbe wa Bodi ya Udhamini wa Chama cha Mbizu Ndg. Vuai Ali Vuai Mwafaka wa Oktoba wa 2001 baina ya CCM na CUF ulioibuka na muafaka wa kuanzishwa kwa chombo ambacho kitawakutanisha wadau wa siasa kwa lengo la kuwa na jukwaa la kukutanisha wadau ili kujadiliana namna ya kuendesha siasa za Tanzania.

“Baraza limetoka mbali lakini chanzo cha Baraza hili litokana na mazungumzo yaliyokuwa yanendele kwa muda mrefu ya Makatibu wa Kuu wa CUF na CCM baadaye zikaundwa kamati wajumbe wakateuliwa kutoka vyama hivyo wakatengeneza document iliyojulikana MUAFAKA wa Oktoba 2001 lengo lake lilikuwa kujenga umoja baada ya maelewano na kuafikiana hatimaye kiundwe chombo kimoja kitakachowakutanisha viongozi mbalimbali wa Vyama vya Siasa ili wapate mahali pakuzungumzia masuala ya kisiasa kwa mustakabari wa Maendeleo ya watanzani”. Alisema Mhe. Vuai.

Mkutano huo wa Baraza la Vyama vya Siasa umefanyika Visiwani Zanzibar kwa Siku tatu kuanzia tarehe 22 hadi 24 ambapo ulitanguliwa na Kikaocha Kamati ya Uongozi lkilichafanyika tarehe 22 katika Ukumbi wa Ofisi ndogo za Bunge Zanzibar na kufuatiwa na mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa ulioshirikisha Makatibu wa Vyama wasiokuwa wajumbe wa Baraza na wawakilishi wa wanawake na kisha kuhitimishwa na mkutano wa uchaguzi wa viongozi wa Kamati za Uongozi wa Baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa Spring Hall uliop katika Hoteli ya Madinat Al Bahr Zanzibar.
Na Aisha Malima-Morogoro

Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Morogoro inaendelea na kazi ya kuziba mashimo na kukarabati barabara kuu ya Morogoro – Iringa ikiwemo katika eneo la Kobogwa lilipo katika hifadhi ya Taifa ya Mikumi ambapo kumetokea shimo kubwa baada ya maji kupita pembezoni mwa Kalvati.

Akizungumza na Kipindi cha TANROADS Mkoa kwa Mkoa leo tarehe 26 Aprili 2024; Meneja wa TANROADS Mkoa wa Morogoro Mhandisi Alinanuswe L. Kyamba amesema kuwa tayari Mkandarasi yupo eneo hilo akiendelea na kazi ambapo mpaka kufika leo usiku kazi hiyo utakuwa imemalizika.

"Mvua zimeendelea kunyesha bila kukatika na jitihada zinaendelea kufanyika kila siku, eneo hili ambalo limeleta taharuki katika barabara hii ya Mikumi. Mashimo yametokea juzi, tukayaziba kidharura lakini unapoziba kidharura mvua zikinyesha tena zinaondoa ule mchanga ambao tumeuweka kwa sababu kipindi hiki cha mvua huwezi kuziba na lami, lami haikubali kipindi cha mvua mpaka jua liwake" Amekaririwa Mhandisi Kyamba na kusisitiza kuwa

“Tunaendelea na kazi ya kuziba mashimo yote kwenye barabara hii kuanzia Msamvu - Mikumi hadi Iringa mpaka tuyamalize kutokana na mvua kubwa kila siku mashimo yanajitokeza juzi hapa kwenye hili Kalvati maji yamepita pembeni yametengeneza shimo kubwa hapa katikati tukaanza kuleta mitambo na nyenzo za kazi, kwa sasa barabara inapitika upande mmoja na upande mwingine kazi inaendelea’’

Kwa upande wake Mhandisi Aloyce Stephen kutoka Kampuni ya Kizawa ya CGI Contractor Ltd inayofanya kazi hiyo amesema kazi imeendelea kufanyika bila kusababisha msongamano wa magari na matarajio ni kwamba magari yaemdelee kuruhusiwa kupita pande zote za barabara bila tatizo lolote.

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa fursa na kuwajali Wakandarasi wazawa ikiwa ni pamoja na kuwapa malipo ya kazi kwa wakati jambo ambalo linawapa nguvu ya kuwa tayari kutekeleza majukumu yao wakati wote hata kwenye kazi za dharura kama hizo.










Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
JESHI la Polisi Mkoani Pwani, limewakamata Diwani wa kata ya Kiromo Mstaafu Hassan Wembe na Askari Mgambo Abdallah Mgeni na baadae kupewa dhamana, kwa kosa la kumshambulia kwa maneno makali, vitisho, dharau na kutishiwa kufungwa pingu Waziri na Mbunge Mstaafu Dkt Shukuru Kawambwa pamoja na Cathbert Enock Madondola huko Kitopeni, wilayani Bagamoyo.


Aidha watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara upelelezi utakapokamilika.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Pwani, Pius Lutumo, alieleza, tarehe 25 april mwaka huu kupitia mitandao ya kijamii ilionekana clip ikimwonesha dkt Kawambwa akishambuliwa kwa maneno na vitisho na kudhalilisha , kufokewa na kutishiwa kufungwa pingu kama mhalifu hali iliyosababisha taharuki kubwa kwa jamii.

"Ukweli ni kuwa April 24 saa 8 mchana dkt Kawambwa na mtu mwingine Cathbert Madondola walishambuliwa kwa maneno, vitisho na kutishiwa kufungwa pingu na diwani Mstaafu kata ya Kiromo Hassan Wembe akiwa na askari mgambo Abdallah Mgeni."alifafanua Lutumo .

Vilevile Kamanda huyo, amemtaka mtu aliyechukua na kusambaza video ya dkt Kawambwa na Cathbert Madondola wakishambuliwa kwa maneno makali na kutishiwa kufungwa pingu na diwani Mstaafu huyo Wembe ajisalimishe kituo cha polisi Bagamoyo mara moja.

"Katika clip iliyokuwa inasambaa mitandaoni iliambatana na maneno yaliyosomeka kuwa Shukuru Kawambwa Waziri wa Miundombinu enzi hizo sasa ni dalali wa viwanja Bagamoyo na mhalifu wa kawaida (common criminal) jambo hili linachunguzwa pia kubaini ukweli" alisema Lutumo.

Alitaja chanzo cha tukio hilo ni magari ya mchanga ya mtuhumiwa Hassan Wembe kuharibu barabara na mashamba ya watu yakipita kwenda kubeba mchanga eneo hilo hali iliyopelekea wananchi kufunga barabara kwa magogo ili kuzuia uharibifu wa barabara.

Lutumo aliwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi, bali wafuate sheria za nchi na kuwatumia viongozi waliopo kwenye maeneo yao kutatua matatizo yao.

Wakati huo huo Dkt Shukuru Kawambwa amesikitishwa na kitendo alichofanyiwa na dwn Mstaafu, Hassan Wembe kwa kumkashifu kuwa ni dalali wa viwanja wakati katika eneo hilo walikuwa wameziba njia na hakukuwa na kesi ya kuuza au kufanya udalali wa viwanja.

"Mimi sijawahi kwenda shamba lolote,kufanya lolote, Wembe kanidhalilisha,na naamini vyombo vya kisheria vitachukua hatua"

Alitoa ufafanuzi kwamba, walikaa katika kikao cha wananchi wa eneo hilo na kuamua kwa asilimia 100 barabara ifungwe isitumike tena kwani wanaharibu miundombinu ya barabara.

"Na mvua zikimalizika atengeneze barabara pia achepushe njia nyingine kupitia eneo lake kwenda barabara kuu ili afanye kazi zake kwa Uhuru kuliko kukera wananchi" alisema Dkt.Kawambwa.

Serikali imesema hadi kufikia Mwezi, Machi 2024 jumla ya vijiji 11,837 sawa na asilimia 96.37 ya vijiji vyote 12,318 vya Tanzania Bara vilikuwa vimeunganishiwa huduma ya umeme.

Hayo yamesema na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Dotto Biteko Bungeni, Jijini Dodoma wakati akisoma Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2024/2025.

Aidha, Dkt. Biteko amesema katika kuimarisha utoaji wa huduma kwa Wananchi vijijini, jumla ya taasisi 63,509 zinazotoa huduma kwa jamii ikiwemo ya elimu, biashara, pampu za maji, vituo vya afya na nyumba za ibada zilikuwa zimeunganishiwa umeme, ikilinganishwa na taasisi 43,925 Mwezi Aprili, 2023.

Vilevile, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kupeleka umeme vitongojini na katika visiwa na maeneo yaliyo mbali na Gridi ya Taifa, vituo vya afya na pampu za maji, wachimbaji wadogo wa madini, viwanda na kilimo, katika shule pamoja na mahakama za mwanzo vijijini.

Dkt. Biteko amesema katika mwaka 2024/25, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itaendelea kupeleka nishati vijijini ili kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi na maendeleo ya kijamii katika maeneo hayo. 

Miradi iliyopangwa kutekelezwa ni pamoja mradi wa kupeleka umeme katika Vitongoji 20,000 ambapo kazi zitakazofanyika ni pamoja na ununuzi wa wakandarasi wa kutekeleza mradi, kufanya usanifu wa kina wa mradi na kuanza ujenzi wa miundombinu ya mradi.

Miradi mingine ambayo itapewa kipaumbele ni pamoja na Mradi wa kupeleka umeme katika Vitongoji 3,060 (vitongoji 15 kila Jimbo) kwa kujenga miundombinu ya mradi, kufunga transfoma na kuunganisha wateja.

Miradi mingine, itakayotekelezwa ni mradi wa Ujazilizi Awamu ya Pili (B); Mradi wa Ujazilizi Awamu ya Pili (C); Mradi wa kupeleka umeme katika maeneo ya Vijijini-Miji; (PERI Urban); Mradi wa kusambaza umeme katika Migodi Midogo, Maeneo ya Kilimo na Viwanda; Mradi wa kupeleka umeme katika minara ya mawasiliano ya simu na mradi wa ufungaji wa mifumo ya umeme jua kwenye makazi yaliyopo Visiwani na yaliyopo mbali na Gridi ya Taifa.

Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, Dkt. Biteko amesema Serikali kwa kushirikiana na Wadau, itaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024 – 2034 kwa kupatia ufumbuzi vikwazo vya matumizi ya nishati hiyo, ikiwemo gharama kubwa, upatikanaji hafifu na uhaba wa miundombinu yake na kukosekana kwa elimu ya kutosha kuhusu madhara ya nishati zisizo safi na salama za kupikia.

Aidha, Mradi wa kusambaza majiko banifu kwenye Kaya zilizopo katika maeneo ya Vijijini na Vijiji-Miji; kutoa ruzuku kwa wazalishaji wa mkaa mbadala kwa ajili ya ununuzi wa mashine zitakazotumika katika uzalishaji wa mkaa huo; kuendelea kushirikiana na Jeshi la Magereza katika ujenzi wa miundombinu ya nishati ya kupikia katika maeneo 211 pamoja na kuendelea na usambazaji wa gesi asilia majumbani, hususan katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Lindi na Pwani.

Na Mwandishi wetu

Kikao cha 23 Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) kinaendelea jijini New York nchini Marekani. Kikao hicho kinahudhuriwa na ujumbe wa Tanzania unaoongozwa na Prof. Hamisi M. Malebo, Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wajumbe wengine wa Tanzania wanaohudhuria mkutano huo ni pamoja na Bi. Zuleikha Tambwe, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Hindu Zarooq Juma, Afisa Mwandamizi wa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Pellage Kauzeni, Afisa Mhifadhi Mkuu wa Wanyamapori katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Agnes Gidna, Kaimu Meneja wa Urithi wa Dunia katika Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Edward Kutandikila, Mwanasheria wa Serikali na Erick J. Kajiru, Afisa Mwandamizi Mkuu katika Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ujumbe wa Tanzania umempongeza Mwenyekiti wa Kikao cha Jukwaa la 23 la Umoja wa Mataifa la Watu wa Asili Hindou Oumarou Ibrahim na Mwenyekiti mwenza kwa kuongoza vizuri kikao cha Jukwaa.

Prof. Hamisi Malebo ameueleza mkutano huo kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kusisitiza msimamo wake wa muda mrefu kwamba hakuna wananchi waliohamishwa kwa nguvu katika tarafa za Ngorongoro na Loliondo kama inavyodaiwa na madai hayo ni ya uongo. Alibainisha kuwa mashauriano na wakazi wa Ngorongoro na Loliondo yalifanyika kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa changamoto za maeneo yote mawili ya hifadhi, mtawalia.

Eneo la kilomita za mraba 4,000 katika eneo la Loliondo ambalo lilikuwa halijawahi kukaliwa na watu na lilipewa hadhi ya hifadhi mwaka 1895 na utawala wa wakoloni wa Kijerumani na limeendelea kuwa hadhi hiyo hadi lilipogawanywa.

Historia iko wazi kuwa, Waamasai na makabila mengine walianza kulivamia eneo hilo baada ya uhuru wa Tanganyika kuanzia mwaka 1961.

Kwa kuzingatia haki za binadamu na maisha ya wananchi waliovamia eneo la Loliondo, Serikali ilitenga eneo la kilometa za mraba 2,500 kwa ajili ya wananchi na kilometa za mraba 1,500 kubakizwa kwa ajili ya uhifadhi wake na kuitwa Pori la Akiba la Pololeti.

Prof. Malebo ameihimiza Sekretarieti ya Jukwaa la Masuala ya Watu wa Asili la Umoja wa Mataifa kutambua na kufahamu ukubwa wa kilometa za mraba 2,500 ulivyo pamoja na mpango mahsusi wa Serikali wa kuweka uwiano wa utekelezaji wa haki za binadamu, uhifadhi na maendeleo ya wananchi.

Prof. Malebo akiwakilisha katika mkutano huo, alieleza kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasikitishwa na utaratibu wa kuandaa mapendekezo ya Jukwaa la Kudumu la Watu wa Asili ambapo mara nyingi maelezo ya Nchi Wanachama hayazingatiwi na huwa ya upande mmoja na hayana uwiano.

Alibainisha kuwa Mataifa Wanachama kama nchi ya Tanzania wameshiriki katika kongamano hili kwa nia njema na kutoa upande wa pili wa maelezo ambao tunaamini unasaidia jukwaa kupata uelewa wa kutosha wa masuala yanayowasilishwa katika mkutano.

Alieleza tabia ya kuchagua na kupendelea katika kuandaa taarifa za mkutano ni hatari na inaleta migawanyiko.

Alitoa wito kwa kongamano kutumia njia ya kutopendelea na yenye uwiano sawa ili kuakisi mada na taarifa zinazowasilishwa katika Mkutano huo.

Ujumbe wa Tanzania umebainisha kuwa Mwandishi wa Kudumu wa Haki za Watu wa Kiasili atakuwa akizuru Tanzania ili kuthibitisha madai kuhusu Ngorongoro na Loliondo, hivyo umelishauri Jukwaa kuwa ni mapema sana kutoa mapendekezo kuhusu Tanzania kabla ya Mwandishi kuwasilisha taarifa ya ziara yake.

Prof. Malebo ameuhakikishia mkutano huo kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaongozwa na utawala wa sheria, kuheshimu haki za binadamu na misingi ya utawala bora.

Kwa hali hiyo, imezingatia haki za binadamu kwa wananchi wake wake wakati ikishughulikia changamoto katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo na Hifadhi ya Ngorongoro.

Na Mwandishi Wetu, Arusha

KAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA), imetoa mafunzo maalumu kwa akina mama lishe 50 wa mkoa wa Arusha kwa lengo la kuwaelimisha namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali ya moto.

Mbali na mafunzo hayo, pia GGML imewagawia mitungi 50 ya gesi ya kupikia kwa ajili ya kuhamasisha akina mama hao kuachana na matumizi ya kuni na mkaa kisha kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi.

Mafunzo hayo yalitolewa jana katika maadhimisho ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika Kitaifa Jijini Arusha kuanzia tarehe Aprili 23 hadi Mei Mosi 2024.

Akizungumza na akina mama lishe hao, Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi amesema wamemua kutoa elimu kwa akina mama hao ili watambue namna ya kupambana na moto majumbani na kuzingatia usalama kwenye maeneo yao ya biashara hasa ikizingatiwa wao ni chanzo kikubwa cha kukutana na watu wengi.

“Tunawafundisha namna ya kupambana na majanga ya moto kwani shughuli zao za kila siku zinahusiana na masuala ya moto na matumizi ya mkaa na gesi.

“Lakini pia ni vema kutambua namna gani mabadiliko ya tabia nchi yanaathiri watu pia namna tabia zetu binafsi zinavyoweza kuchangia kuachana na ukataji hovyo wa miti,” amesema.

Amesema athari za mabadiliko ya tabia nchi, zinamuathiri kila mmoja bila kujali, cheo, mkubwa au mdogo hivyo ni vema kila mmoja kuzingatia matumizi ya nishati safi ili kuondokana na majanga yatokanayo na mabadiliko hayo.

“Tumeandaa elimu hii kuona namna ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa sababu ukataji wa miti ukikithiri unasababisha mmonyoko wa ardhi, mafuriko na ongezeko la joto duniani.

“Matumizi ya mkaa au kuharibu vyanzo mbalimbali ambavyo vinaweza kusabababisha athari kwenye mazingira na kusababisha mafuriko hata kwenye maeneo yetu ya uchimbaji,” amesema.

Kwa upande wa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi amesema katika mafunzo hayo, wamewafundisha akina mama hao namna salama ya kutumia nishati ya gesi na kuwasisitiza kuondokana na matumizi ya mkaa.

“Lakini pia kwenye banda letu tumeendelea kupokea wageni wanaopenda kujifunza namna ya kupambana na majanga ya moto kwa sababu asilimia kubwa wanauelewa mdogo namna ya kukabiliana na majanga ya moto majumbani,” amesema na kuongeza;

“Watu wengi hawajui njia za awali za kupata msaada wa kuzima moto, sisi tunatoa mafunzo hayo, kuna vifaa vya kawaida ambavyo mama yeyote anavyo nyumbani, mfano ndoo ya maji, taulo, kanga au kitenge vilivyolowekwa kwenye maji, ni vifaa vya kawaida ambavyo unaweza kutumia kuzima moto hivyo tunaendelea kuwaribisha kwenye mabanda yetu,” alisema.

Wakati huo huo Mkaguzi wa afya ya mazingira ya kazi kutoka OSHA, Elizabeth Mtile amewasisitiza akina mama hao kuzingatia umuhimu wa kufuata sheria na miongozo mbalimbali ya usalama na afya katika maeneo ya kazi.

“Kauli mbiu yetu inayosema athari za mabadiliko ya tabia nchi katika usalama na afya kazini, inalenga kudhibiti majanga na mabadiliko haya ya tabia nchi kwa kushirikisha kila kundi kwenye jamii kwani athari hizi zinatugusa sisi sote,” amesema.

Mmoja wa akina mama lishe hao, Prinsila Kwai aliishukuru GGML na OSHA kwa kupatia mafunzo hayo kwani yanaenda kuwa chachu ya mabadiliko kwao na kwa wale wanaowazunguka.

“Kwa kweli tunashukuru sana kwa shughuli zetu za kila siku zinahusiana na moto hivyo mafunzo haya yatatusaidia sana namna ya kukabiliana na mlipuko labda wa gesi,” amesema.
 

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.
 

Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi akimgawia mtungi wa gesi ya kupikia mmoja wa akina mama lishe waliopatiwa mafunzo ya namna ya kuzima majanga ya moto wakati wanapoendelea na shughuli zao za kupika. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha ambao pia wote waligawiwa mitungi ya gesi.
 

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akiwaonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.
 

Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk. Kiva Mvungi (kulia) akizungumza na akina  mama lishe kuwaeleza namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama wakati Wimbo wa Taifa wa Tanzania na ule wa Afrika Mashariki ukiimbwa katika Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kushuka kwenye gari Maalum la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.

ORB OF DESTINY ni mchezo wa sloti kutoka kwa Hacksaw Gaming. Katika mchezo huu wa kasino ya mtandaoni, unaleta mshangao mzuri. Kuna Wilds zenye nguvu na mizunguko ya bure inayokuja na ushindi wa hali ya juu. Jisajili Meridianbet na Ushinde kirahisi kila unapocheza kasino.

Orb of Destiny ni mchezo wenye mistari ya 14 ambao hauwezi kubadilishwa. Ili kushinda, lazima uunganishe alama tatu au zaidi za kufanana kwenye mstari wa malipo.

Kila mchanganyiko wa kushinda unahesabiwa kutoka kushoto kwenda kulia, kuanzia na safu ya kwanza upande wa kushoto.

Unaweza kupata ushindi mmoja kwa kila mstari wa kulipa. Ikiwa una mchanganyiko zaidi ya moja kwenye mstari wa kulipa, utapewa ushindi wa thamani kubwa zaidi.

Inawezekana kukusanya ushindi wakati unawaunganisha kwenye mistari ya kulipa zaidi ya moja kwa wakati mmoja. Katika sehemu ya Bet, kuna mishale ya juu na chini ambayo unaweza kutumia kuweka thamani ya dau kwa kila mzunguko.

Katika mchezo huu wa kasino ya mtandaoni kuna chaguo la kucheza moja kwa moja ambalo unaweza kuliwasha wakati wowote. Kupitia chaguo hili, unaweza kurekebisha hadi mizunguko 1,000.

Ikiwa unapenda mchezo wa haraka zaidi, tunayo suluhisho kwako. Mchezo una spin za haraka au za haraka sana ambazo unaweza kuziwezesha wakati wowote.

Alama za Ushindi za Kasino Ya Mtandaoni.
Katika suala la alama za ushindi kwenye mchezo huu wa kasino ya mtandaoni, alama ya chini zaidi ni vifurushi vya kubebea. Utaviona moja, mbili, tatu, nne, na tano. Thamani yao ya malipo imepangwa kwa mpangilio huo.

Alama zote nyingine za msingi zinawakilishwa na kadi zinazotumiwa kwa tarot.

Kadi ya bluu, kijani, na zambarau zina thamani sawa ya malipo. Ikiwa utawaunganisha simba sita hawa kwenye mchanganyiko wa kushinda, utapata mara 15 ya dau lako.

Kisha utaona kadi nyekundu ambayo inatoa malipo makubwa zaidi. Ikiwa utawaunganisha simba sita hawa kwenye mchanganyiko wa kushinda, utapata mara 20 ya dau lako.

Malipo makubwa zaidi kati ya alama za msingi ni kadi yenye Jua. Ikiwa utawaunganisha simba sita hawa kwenye mzunguko wa ushindi, utapata mara 25 ya dau lako.

NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz
Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla  iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.













Top News