THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.

  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com






Waziri mkuu Pinda azindua mradi wa kuimarisha halmashauri za miji 18 Tanzania bara

Waziri mkuu Mizengo Pinda akikata utepe katika vitabu kuashiria kuzinduliwa kwa mradi wa kuimarisha halmashauri za miji 18 Tanzania bara,Uzinduzi huo uliofanyika mjini Moshi.Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi, Hawa Ghasia na kulia ni Mwakilishi wa benki ya dunia,mkurugenzi mkazi Philippe Dongies wakishuhudia.
Waziri mkuu Mizengo Pinda akiwahutubia washiriki wa warsha ya uzinduzi wa mradi wa kuimarisha halmashauri za miji 18 Tanzania bara uliofanyika mjini Moshi.
Washiri wa warsha hiyo.


mapitio ya magazeti leo


Kili Music Tour 2013 kuanzia Dodoma jumamosi juni 22

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) chini ya Bia yake ya Kilimanjaro, inataraji kuanza rasmi tamasha kubwa la muziki lijulikanalo kama ‘Kili Music Tour’ wikiendi hii katika mji wa Dodoma.

Tamasha hii kubwa linatarajiwa kuanza siku ya Jumamosi ya tarehe 22 Juni, 2013 mjini Dodoma kwenye viwanja vya Jamhuri na litajumuisha wasaniii 8 ambao ni Ally Kiba, Ommy Dimpoz, Professor J, Ben Pol, Lady Jay Dee, Lynex, Roma na Kala Jeremiah.

Mwaka huu Bia ya Kilimanjaro imebadilisha utaratibu wa tamasha hili la muziki ambalo lilikuwa linajulikana kama KTMA Winners Tour na lilikuwa likijumuisha wasanii walioshinda tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards pekee.

Mwaka huu bia ya Kilimanjaro imebadilisha jina la tamasha kuwa Kili Music Tour na litashirikisha wasanii wote kwa ujumla na sio washindi wa tuzo za KTMA pekee.

“Kili Music Tour imepanua wigo wake kwa kushirikisha wasanii walioshinda tuzo, wasanii waliokuwa kwenye mapendekezo ya tuzo na wasanii ambao hawakushiriki kabisa kwenye tuzo lakini wako juu kwenye tasnia ya muziki nchini. 

Hii ni kwenye kuhakikisha kuwa mashabiki wa muziki wanapelekewa wasanii wanaowapenda kwenye mikoa yako bila kubagua. Mwaka huu matamasha yameongezeka kutoka sita mwaka jana na kuwa nane.

Kili inaelewa ni jinsi gani watanzania wanajivunia mambo ya kitanzania kama muziki wetu wa bongo flava, dansi yetu ya kiduku, kandanda letu lenye ushabiki wa simba na yanga, lugha yetu ya kipekee na bia yetu ya Kilimanjaro inayowapa bonge la kiburudisho .

Ndio maana tumeongeza wigo wa Tamasha kama ishara ya shukurani kwa jinsi watanzania wanavyojivunia mambo ya kikwetu kwetu.” Alisema Bwana George Kavishe Meneja wa bia ya Kilimanjaro.

Msanii aliyebobea wa bongo flava ajulikanaye kama Kala Jeremiah naye alisema “ mwaka huu mashabiki wategemee kupata vionjo ambavyo hawajawai kuviona kwani mimi na wasanii wenzangu tumejipanga kikamilifu kuhakikish kuwa hatuwaangushi mashabiki wetu na kuwa tunawapa bonge la kiburudisho!” 


Benki ya BADEA yaisaidia Serikali ya Tanzania katika miradi ya maji na kituo cha hesabu

Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa akiongea jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) Abdelaziz Khelef wakati wa utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa (kushoto) akimshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) Abdelaziz Khelef mara baada ya kumalizika utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe akipongeza Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Kuli ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) Abdelaziz Khelef.
Baadhi ya maofisa kutoka Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) wakifuatilia utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.Picha na Anna Nkinda - Maelezo.


Mpigie Kura yao Mshiriki Nando ili aweze endelea kubaki ndani ya jumba la Big Brother


Furaha ya burudani ya miaka ilee sasa imerejea

Furaha ya burudani ya miaka ilee sasa imerejea. Melegendari sasa wamekiri kuwa walichokikosa kwa muda mrefu, sasa kinapatikana isumba lounge -jollies club kila ijumaa na j'mosi. Ni katika night of the legends na DJ John Dillinga aka The Legend is Back, DJ Fast Eddy na DJ Young Kelvin. Njoo ujumuike na malegendari wenzako ukumbukie wakati muziki ukiitwa muziki. Milango iko wazi saa 3 usiku, kiingilio 10,000/-. Karibu sana. 4 more info or comments like facebook page @www.facebook.com/pages/DJ-JD or follow instagram @DJJDTHELEGEND


RAIS KIKWETE AREJEA NCHINI BAADA YA ZIARA YA KIKAZI NCHINI UINGEREZA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza kwa makini maelezo aliyokuwa akipewa na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda mara tu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akitokea nchini Uingereza. Rais Kikwete alirejea nchini tarehe 18.6.2013 usiku baada ya ziara ya kikazi nchini Uingereza. PICHA NA JOHN LUKUWI


New UNHCR report says global forced displacement at an 18-year high ;Tanzania hosting the 5 th largest refugee camp




SHUKRANI

Familia ya Bw. Thomas Martin Kiama, aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, kwa mara nyingine tena, kwa moyo mkunjufu tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa ndugu, jamaa, marafiki, wafanyakazi wenzetu na wote wenye mapenzi mema kwa kutufariji kwa hali na mali wakati wa msiba wa mpendwa mama, dada, bibi, rafiki na mke Victoria Thomas Kiama uliotokea tarehe 11 Mei, 2013.

Kwa upendo, tunawaomba wote kujumuika nasi katika Misa ya Shukrani itakayofanyika Jumamosi tarehe 22 Juni, 2013 katika Kanisa Anglikana la Mt. Albano, lilipo karibu na Posta Mpya saa 2 asubuhi, na baadae katika chakula cha mchana nyumbani, Mtaa wa Bongoyo, Oysterbay karibu na Ubalozi wa Kenya.

Tunamuomba Mungu wa Mbinguni aipumzishe roho ya Mpendwa wetu katika amani ya milele.

Amina.


WAJUMBE WA ALAT RUVUMA WASHAURI KUWEPO KWA MIPANGO YA MUDA MREFU

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma akitoa maelezo kwa mkuuu wa Wilaya ya Songea juu ya kikao chao cha ALAT ambacho wamejiwekea utaratibu wa kukutana kila baada ya miezi mitatu kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa ilani ya CCM.
Toka kulia kwako ni Katibu wa ALAT Mkoa wa Ruvuma Mohemed Maje, Makamu mwenyekiti wa ALAT ambaye pia ni Menyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Stevini Nana, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho na Naibu meya wa Manispaa ya Songea Wiloni Kapinga wakipitia kablasha la kikao cha ALAT.Picha na Demasho Blog.


MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA BARANI AFRIKA YANAYOENDELEA NCHINI GHANA

Afisa Tawala Mwandamizi wa Wizara ya Fedha Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali Bw. Merkion Ndofi akimkaribisha mwananchi wa Ghana katika banda la Wizara ya Fedha.
Bw. William Ghump amabaye ni Ofisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi wa Wizara ya Fedha na Mkurungezi wa Utawala na Utumishi Bw. Peter Mapigano wa Benki ya Posta Tanzania pamoja Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma wakipanga mkakati wa uelimishaji umma katika banda la Wizara ya fedha.
Waziri wa Utumishi wa Umma ,Ofisi ya Rais Bi. Celina Kombani na Katibu Mkuu Bw. George Yambesi walipotembelea banda la Wizara ya Fedha hapa nchini Ghana.
Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi Ingiahedi Mduma akifafanua jambo kwa Bw. Eugene Koranteng Henaku wa Umoja wa Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Serilkali za Mitaa Nchini Ghana.


Warembo wa Redd's Miss Tanga 2013 watembelea Mapango ya Amboni jijini humo

Washiriki wa shindano la Redd's Miss Tanga 2013 wakiwa katika mapango ya Amboni jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya kutangaza utalii uliopo katika mkoa wa Tanga.Shindano lao litafanyika katika uwanja wa Mkwakwani Mjini Tanga siku ya Ijumaa Juni 22,2013.
Warembo wakiendelea na safari yao ndani ya Mapango hayo.
Washiriki wa shindano la Redd's Miss Tanga 2013 wakiwa nje ya mapango ya Amboni jijini Tanga ambako walitembelea ikiwa ni sehemu ya kutangaza utalii uliopo katika mkoa wa Tanga.Shindano lao litafanyika katika uwanja wa Mkwakwani Mjini Tanga siku ya Ijumaa Juni 22,2013.


mama Kkikwete apongezwa kwa kuendeleza soka nchini

Na Anna Nkinda – Maelezo
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amepongezwa kwa jitihada zake za kuinua sekta ya michezo nchini   jambo ambalo limewafanya  vijana wengi kujipata ajira katika fani hiyo.
Pongezi hizo zimetolewa jana na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Lindi  (LIREFA) Francis Ndulane wakati wachezaji wa timu ya Kariakoo ya mkoa huo walipozitembelea ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA)  zilizopo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Ndulane alisema kuwa mchango unaotolewa na  Mama Kikwete umewapa hari na kuwatia  moyo vijana wengi na hivyo kuweza kuendeleza sekta ya michezo mkoani humo.
Alisema kuwa hapa nchini vijana wengi wana vipaji mbalimbali, lakini hawana watu wa kuwaendeleza, hivyo alimshukuru kwa jitihada zake za kuwaendeleza katika sekta hiyo na hivi sasa  wanaamini  kuwa wataweza kujiajiri na kuweza kuzisaidia familia zao.
Kwa upande wake Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA aliwapongeza wachezaji hao kwa juhudi kubwa wanayoifanya katika soka hadi kufikia hatua ya kushiriki ligi ya taifa ya mabingwa wa mkoa ngazi ya taifa na kufikia hatua ya nane bora.
Naye Mwenyekiti wa timu hiyo Abdalah Livemba aliwashukuru Mama Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe kwa moyo walionao wa kuisaidia timu hiyo hadi kufikia  hapo ilipo.
Alimuomba kuwatafutia mdhamini ili aweze kuwasaidia  kubeba mzigo mkubwa wa kuitunza timu hiyo ambao unaelekea kuwalemea.
Mama Kikwete aliikabidhi timu hiyo zawadi za  viatu pea 29, jezi seti mbili ambazo ni 32, mipira mitatu, pampu moja  na  soksi  pea 16.
Timu ya Kariakoo inashiriki mashindano ya ligi ya mabingwa mkoa ngazi ya Taifa ambayo yalianza tarehe 12/6/2013 kwa kuzishirikisha  timu 28 kutoka nchi nzima wao wamebaki kati ya timu nane na leo wanapambana na Friends Rangers ya mkoa wa Dar es Salaam mchezo utakaofanyika katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam.






Zantel yazindua huduma ya taarifa za kilimo kwenye simu za mikononi.


 Mkurugenzi wa mazao wa wizara ya kilimo, chakula na ushirika, Dkt.Mshindo Msolla akisisitiza jambo wakati wa kuzindua huduma ya Z-KILIMO
 Wafabyakazi wa Zantel wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa wizara ya kilimo.

Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel, kwa kushirikiana na wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na kampuni ya Sibesonke leo wamezindua huduma mpya ya kutoa taarifa kuhusu kilimo kupitia simu za mikononi.
Huduma hiyo mpya inayofahamika kama,Z-KILIMO,itawawezesha wakulima nchini Tanzania kupata taarifa za papo kwa pao na uhakika kuhusu njia za kuendesha kilimo cha kisasa kwenye simu zao za mikononi.
Kupitia huduma hii ya Z-KILIMO, wakulima nchini, hata wale walio vijijini wataweza kupata taarifa muhimu za namna ya kuendesha kilimo cha kisasa na hivyo kuongeza uzalishaji na kukuza sekta nzima ya  kilimo. Akizungumza kwenye uzinduzi wa huduma hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Rasirimali watu cha Zantel, Francis Kiaga, amesema kwa kupitia huduma hii wakulima nchini watapata fursa ya kipekee kupata taarifa kuhusu kilimo moja kwa moja kupitia simu zao.

“Kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu, na kinachangia sana kwenye kukuza na kuchangia uchumi wa nchi yetu, na huduma hii imekuja wakati muafaka katika kuendeleza juhudi hizo, lakini pia kuwapa wakulima umuhimu wa huduma ya simu katika namna wanayoihitaji zaidi’ alisema Kiaga.

Akielezea zaidi huduma hiyo Kiaga alisema itawasaidia zaidi wakulima katika kuokoa muda ambao zamani waliupoteza katika kupata taarifa kuhusu kilimo, na pia kuwaongezea uzalishaji wa mazao yao.
Huduma ya Z-KILIMO pia itawapa wakulima taarifa kuhusu maandilizi ya ardhi, aina za mbolea, aina za mazao, aina za mifugo, aina ya magonjwa yanayoshambulia mazao, upaliliaji, taarifa za usafiri, hali ya hewa pamoja na sehemu ya majadiliano baina ya wakulima.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kilimo wa wizara, Daktari Mshindo Msola, alielezea kufurahishwa kwake na huduma akisema itasaidia kufungua fursa zaidi kwa wakulima nchini. ‘Kupitia huduma hii, wakulima sasa wataweza kuboresha mbinu zao za kilimo katika hatua zote za kilimo na hivyo kuongeza uzalishaji’ alisema Dkt Msola.
Nao kampuni ya Sibesonke, ambao wameingia ushirikiano wa kiteknolojia na wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na wizara ya maenedeleo ya Mifugo na Uvuvi, ukiwa na lengo la uwafikia watanzania wakulima kuwapa taarifa muhimu za kilimo kwenye simu zao.

“Sibesonke ina furaha kwa kuwezesha watanzania kufaidika na teknolojia hii kupitia mtandao wa Zantel’ alisema Daktari Uwe Schwarz, Mkurugenzi Mkuu wa Sibesonke. “Kampuni ya Zantel imeonyesha dhamira ya dhati katika kuhakikisha teknoljia hii inawafaidisha watanzania wote kwa mtandao wake ulioenea nchi nzima’ alisiistiza Daktari Schwarz.

Wakulima wanaweza kujiunga na huduma hii kwa kubonyeza *149*50#, ambapo wataweza kupata maelekezo ya kutumia huduma hii.  


UMOJA WA WAMILIKI WA MALORI TANZANIA WALALAMIKIA KUPANDISHWA KWA BEI ZA BIMA

 Msemamaji wa Umoja wa wamiliki wa Malori Tanzania, Bwana Elias Lukumay akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na malalamiko ya kampuni yake kuhusiana na ongezeko la bima. Kulia kwake ni Makamu mwenyekiti wa TATOA, Bi Angellina Ngalula.
 Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Malori Tanzania, Bi Angellina Ngalula akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na malalamiko ya umoja wao ya kupanda kwa bei za bima kwa asilimia 400. Kushoto kwake ni msemaji wa TATOA, Bwana Elias Lukumay.
=========  ========  =======  =========
UMOJA WA WAMILIKI WA MALORI TANZANIA WALALAMIKIA KUPANDISHWA KWA BEI ZA BIMA

Umoja cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA) umelalamikia ongezeko la bei za bima, ukisema hazijazingatia uhalisia wa soko, pamoja na kukosa uhalali kwa kuwa hazijashirikisha wadau wa sekta ya usafiri pamoja na jamii kwa ujumla.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, msemaji wa TATOA Bwana Elias Lukumay, alisema wanasikitishwa na mamlaka ya uthibiti wa bima Tanzania (TIRA) kuongeza malipo ya bima kwa asilimia 400 bila kutoa sababu za msingi lakini pia bila kushirikisha wadau.

‘Majaribio yetu ya kuzungumza na TIRA yameshindika baada ya TIRA kutojibu barua wala mawasiliano rasmi ya kukutana nao, tofauti na makubalino yetu ya kikao cha mwezi wa pili, kati yetu na wao ambapo tulikubaliana kuwa na kikao kabla ya mazungumzo baina ya wadau na umma juu ya swala hili’ alisema Lukumay.

Akielezea zaidi kuhusu malalamiko hayo, Lukumay alisema vigezo maalumu vya kupandisha bei hizo haviko bayana lakini pia ushindani wa biashara haukuzingatiwa. ‘TATOA inaamini kuna njia nyingi za kufata ili kupandisha bei, lakini kubwa zaidi ni kuacha soko lijiendeshe lenyewe, kwani tuko kwenye soko huria’ alisema Lukumay.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa TATOA, Bi Angellina Ngalula, alisema ongezeko hili la bei ni kubwa mno kwa mara moja na litapunguza ushindani wa makampuni ya usafirishaji ya ndani, lakini pia litaongeza bei za usafirishaji kwa kiwango kikubwa sana na hivyo kuumiza uchumi wa nchi na mwananchi wa kawaida ataathirika kwa bei za bidhaa kupanda.

‘Sababu za TIRA kupandisha bei sio za msingi, sababu kama udanganyifu na kuongezeka kwa kesi za bima pamoja na ajali za barabarani, sio sababu tosha za kupandisha bima kwani kufanya hivyo kutaongeza malalamiko zaidi, na pia kuwavunja moyo wateja waaminifu’ alisema Bi Ngalula.

Bi Angellina pia alitoa wito kwa wahusika, yaani TIRA, kuacha tamaa na kutokuendeshwa na genge la makampuni ya bima na kurudi kwenye meza ya majadiliano ili kuweza kupata muafaka kwa mujibu wa taratibu na sheria za nchi kwa maendeleo ya taifa.

‘Bila TIRA kurudi kwenye meza ya majadiliano TATOA itabidi ichukue hatua mbadala kama kwenda mahakamani na kugomea bei hizi mpya, jambo ambalo litasababisha usumbufu kwenye uchumi wetu’ alisitiza Bi Ngalula.


miondoko ya kumeremeta kwenye mnuso


mkataa kwao mtumwa


ngoma azipendazo ankal


Watanzania wa Nurnberg katika Afrika Festival Nurnberg,UJERUMANI

Watanzania waishio kwenye mji wa Nurnberg na sehemu za jirani na mji huo nchini Ujerumani,wameshiriki vyema Maonyesho ya Afrika Festival Nurnberg iliyofanyika kuanzia tarehe 13.-16. Juni 2013 mjini huo.Wageni mbali mbali walifanikiwa kutembelea Banda la Tanzania kujionea mambo mbali mbali yaliopo nchini kwetu.
Bwana Ramadhani Barungi akitoa maelezo kwa mgeni.
pilikapilika katika Banda la Tanzania.
Wageni wakionja maandazi na chapati.
Bwana Mukada Kidawa kushoto na Bwana Erick Morro, mwenyekiti wa Watanzania Nurnberg wakipokea msaada wa vifaa vya michezo na muziki kwa ajili ya Taasisi ya Talent Search and Empowerment.




OXFAM KWA KUPITIA KAMPENI YA GROW YATOA WITO KWA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI KUWEKEZA KWA WAKULIMA WADOGO NA WA KATI

IMG_7191
Mwanasheria –Mshauri Mwelekezi katika Masuala ya Haki za Ardhi - Emmanuel Massawe akifafanua jambo kwa wageni waalikwa wakati wa hafla ya kuwatangaza rasmi mabalozi wa OXFAM katika Kampeni ya GROW nchini itakayowezesha mfumo wa chakula kuwa wa haki na salama.

Taasisi isiyo ya kiserikali ya OXFAM kwa kupitia Kampeni yake ya GROW imewakutanisha pamoja masupa staa saba wa Tanzania wakiwemo Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee pamoja na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mh. Shy-Rose Bhanji kufanyakazi pamoja na vikundi vya wanawake wajasiriamali na wazalishaji, kwa lengo la kuhakikisha hakuna mtanzania atakayeteseka kwa njaa wakati mbinu za kilimo zinaweza kufanikiwa.

Akizungumza wakati wa kuwatambulisha rasmi mabalozi wa OXFAM kupitia kampeni hiyo, mmoja wa mabalozi hao Bi. Khadija Mwanamboka amesema kilimo sio tu ni sekta endelevu nchini Tanzania bali pia ni Nyanja inayowezesha kupatikana kwa chakula kwa familia na akiba ya chakula kwa taifa kwa kuwa asilimia 80 ya wajasiriamali nchini ni wakulima.

Nchini Tanzania takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya wajasiriamali wanawake wanajihusisha na kilimo kikiwepo cha mbogamboga na matunda.

Aidha kampeni hiyo inakusudia kuendeleza na kukuza uzalishaji utakaoyafanya mazao hayo ya kilimo kuwa na bei muafaka kwa faida ya wakulima hao wa chini na wa kati.
IMG_7195
Naibu Mkurugenzi Mkazi OXFAM-Justin Morgan akziungumza na wageni waalikwa namna kampeni hiyo itakavyofanya kazi zake za uhamasishaji hapa nchini.


Mahojiano na binti "Mtanzania" aliyekamatwa na madawa ya kulevya Misri

KUMRADHI WADAU: LUGHA ILIYOTUMIKA KWENYE HABARI HII NI YA KIARABU NA KINA SIE LUGHA HIYO NI NOT RICABO,LAKINI MAHOJIANO NA MSICHANA HUYO AMBAYE NI MTANZANIA YAPO KWA LUGHA YA KIMOMBO,HIVYO MSIACHE KUANGALIA VIDEO HII MPAKA MWISHO.


Balozi Seif Ali Iddi atembelea mradi wa Barabara ya Cheju – Jendele – Kaebeona,Zanzibar

Msimamizi wa Mradi wa Barabara tatu za Vijijini za Unguja kutoka Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano Mhandishi Suleiman Abdulla Ali akimpatia maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyetembelea mradi huo katika Barabara ya Cheju – Jendele – Kaebeona. Kati kati yao aliyevaa kofia ya Kiua ni Waziri wa Wizara hiyo Rasdhid Seif na pembeni ya Mhandisi Suleiman ni Mshauri Muelekezi waMradi huo Kutoka Kampuni ya Newtech Consulting Group ya Nchini Sudan El- Tayeb Rabah Mohammed.
Mshauri Muelekezi waMradi huo Kutoka Kampuni ya Newtech Consulting Group ya Nchini Sudan El- Tayeb Rabah Mohammed akimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif ujenzi wa bara bara zenye kiwango katika mradi wa bara bara tatu za Vijiji za Unguja huko Cheju Wilaya ya Kati, Mkoa Kusini Unguja. Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.


MRISHO MPOTO NA MJOMBA BAND KUHAMASISHA KAMPENI YA KUNAWA MIKONO NA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA MIKOA MITANO NCHINI

IMG_1058
   Msanii wa kughani na kuimba nyimbo za asili Mrisho Mpoto ambaye pia ni Mkurugenzi wa ‘Mjomba Band’ akizungumza na Mhariri wa Mo Blog Lemmy Hipolite (kushoto) kuhusiana na kampeni ya kunawa mikono kwa sabuni na ujenzi wa vyoo bora ili kuepukana na maradhi yanayosababishwa na uchafu. Kampeni hiyo itafanyika katika mikoa mitano hapa nchini ikianzia na Dodoma, Mara, Njombe. Rukwa na Tanga.

Mwanamuziki na mghani maarufu wa nyimbo za asili ya nyumbani Mrisho Mpoto amewataka wasanii na wanamuziki wote nchini Tanzania kuwa kitu kimoja kwa kujenga ushirikiano na muungano ili kuweza kuufikisha muziki wa hapa nyumbani katika malengo ya kimataifa.

Akizungumza na Mtandao Maarufu wa Habari jijini Dar es Salaam, Msanii huyo Mrisho Mpoto maarufu kama ‘Mjomba’ amesema katika kujulikana kwenye michezo kama inayofanyika kwa sasa, vikundi vya uhamasishaji vinavyotumia sanaa ya asili ni muhimu kutumika ili kuweza kukuza lugha pamoja na utamaduni wa nyumbani.

Amesema ili kufanikisha usafi wa mazingira ikiwemo siku ya kimataifa ya kunawa mikono ni muhimu jamii ya watanzania kuzingatia usafi ili kuepukana na magonjwa ya kuambukiza yanayotokana na uchafu unaoambukiza maradhi yanayotokana na uchafu.

Aidha amesisitiza jamii kujenga utamaduni wa kujenga na kutumia vyoo bora na kuboresha mzingira kwa ujumla ili kuhakikisha elimu hiyo inawafikia walengwa kwa kubadili tabia na njia mbadala za mawasiliano kuhusu elimu hiyo.

Amesema mwaka 2010 aslimia 9 tu ya wananchi waishio vijijini na asilimia 22 ya wananchi waishio mijini waliweza kupata huduma bora za usafi wa mazingira.

Katika kampeni hiyo Mrisho Mpoto na kundi lake la Mjomba Band wataanzia mikoa ya Dodoma, Mara, Njombe, Rukwa na Tanga kabla ya kuendelea mikoa mingine ambayo kwa pamoja na watashirikianana na Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii.


Mafunzo kwa Wakufunzi kutoka VETA na Taasisi za Teknolojia yafanyika jijini Dar

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Eng. Ngosi Mwihava akifungua mafunzo kwa wakufunzi wa Vyuo vya ufundi na Taasisi za Teknolojia kutoka Zanzibar na Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Kigoma na Morogoro. Mafunzo hayo ya siku nne yamefunguliwa leo katika Hotel ya Blue Pearly jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mazingira - Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Julius Ningu.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Eng. Ngosi Mwihava (Hayupo pichani)mafunzo hayo ni maalum kwa wakufunzi wa Vyuo vya ufundi na Taasisi za Teknolojia kutoka Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Kigoma, Morogoro na Zanzibar. Mafunzo hayo ya siku nne yamefunguliwa leo katika Hotel ya Blue Pearly jijini Dar es Salaam yanalenga kukuza uelewa wa kutambua gesi haribifu kwa mazingira.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Eng. Ngosi Mwihava (waliokaa wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo.


Jeshi la polisi Jijini arusha lakitaka Chama cha Chadema kutofanya shughuli zozote kwenye viwanja vya Soweto

Mahmoud Ahmad,Arusha

Jeshi la polisi limekipiga marufuku chama cha demokrasia na maendelo (CHADEMA) kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo huku mabomu yakirindima uwanjani hapo.

Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani hapa Liberatus Sabas alisema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi. Kamanda Sabas alisema kuwa kwa hiyo jeshi hilo limewataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini si kwenye viwanja hivyo.

Hali kwenye viwanja hivyo imekuwa ya pilika pilika tangia juzi kwa wafuasi wa chama hicho kujikusanya tokea asubuhi hadi jioni kwa madai ya kuomboleza tukio la bomu la kurushwa kwa mkono lililotokea uwanjani hapo juzi.

Hata hivyo viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo walikuwa wamukusanyana kwenye uwanja huo hali iliyoendelea kuleta mvutano kati ya viongozi wa jeshi la polisi na wafuasi hao baada ya kukaidi amri ya jeshi hilo mabomu yalirindima uwanjani hapo.

Baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho walikuwepo uwanjani hapo akiwemo mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika,Ezekia Wenje na wabunge mbali mbali wa chama hicho walikuwa kwenye kikao cha bunge kinachoendelea hali hiyo imeliweka jiji hili kusimama shughuli zake kutokana na mabomu hayo.


taarifa ya msiba

FAMILIA YA MAREHEMU MWALIMU. PHILIP NHIGULA WA MALYA MWANZA WANASIKITIKA KUONDOKEWA KWA BABA YAO MPENZI MWALIMU PHILIP NHIGULA (86) ALIYEFARIKI TAREHE 17/06/2013 SAA SABA MCHANA HOSIPITALI YA TAIFA MUHIMBILI AMBAKO MWILI UMEHIFADHIWA.


SHUGHULI ZOTE ZA MIPANGO YA MAZISHI ZINAFANYIKA KIJITONYAMA, DAR ES SALAAM NYUMBANI KWA MTOTO WA MAREHEMU MRS. SAYAYI. MAZISHI YATAFANYIKA JUMAMOSI TAREHE 22/06/2013 MAKABURI YA KINONDONI.

TAARIFA ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.


Taarifa toka Shirikisho la Soka (TFF) leo


UZINDUZI WA MFUMO WA MAWASILIANO WA KUFIKISHA TAARIFA ZA HALI YA HEW NA USHAURI KWA WAKULIMA KUTIA SIMU YA MKONONI UITWAO ‘FARMSMS’, WILAYANI LUSHOTO, 14 Juni 2013

Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini kwa kushirikiana na Chuo cha Sokoine cha Kilimo (SUA) chini ya ufadhili wa shirika la ‘Climate Change Agriculture and Food Security CCAFS’ linalotekeleza mradi wa elimu ya asili katika utoaji wa utabiri wa hali ya hewa katika wilaya ya Lushoto.

Akizungumza katika uzinduzi huo,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania , Dkt Agnes Kijazi alisema utekelezaji wa mradi huu ulianza Agost 2012 na unatarajiwa kuisha mwezi Desemba 2013 ambapo watabiri wa asili wapatao 27 wamehusishwa.

Dkt Kijazi alisema kwa vile wilaya ya Lushoto hupata misimu miwili ya mvua kwa mwaka yaani Vuli na Masika, watabiri hao waasili walihusihwa katika kutoa utabiri wa Vuli 2012 na Masika 2013, na kubaini kushabihiana kwa kiasi kikubwa kwa utabiri wa kisayansi uliotolewa na TMA pamoja na ule wa asili, viashiria vya asili vinavyotumika ni pamoja na wadudu,mimea,wanyama na upepo.

Aliendelea lusema katika kuhakikisha kwamba utabiri wa hali ya hewa unawafikia wakulima kwa wakati ndipo TMA na SUA wameanzisha mfumo wa FarmSMS ambapo uendeshwaji wake utakuwa TMA.

Akizundua rasmi mfumo huo, Kwa niaba ya MKuu wa Wilaya ya Lushoto Bwana Charles Moshi aliwashukuru TMA pamoja na SUA kwa kuwakumbuka wakulima wa Wilaya yake, kwa vile Wilaya ya Lushoto ni moja ya eneo lililoathiriwa na mabadiliko ya tabia nchi kwa kupata upungufu wa mvua katika maeneo mengi, hivyo natarajia kwa mfumo huu wakulima wataweza kupata taarifa sahihi na kwa wakati, Bw. Moshi alisema wazee wa lushoto wamekuwa wakitoa utabiri wa hali ya hewa kwa njia ya asili tangu zamani, ni faraja yetu kuona sasa watabiri wa asili wataweza kuungana na watabiri wa kisayansi katika kutoa utabiri wa eneo husika katika wilaya yetu, hali hii isaidia kuweka kumbukumbu za viashiria vya asili vya utabiri wa hali ya hewa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Aliendelea kuwashukuru wa TMA kwa kuweka kituo cha hali ya hewa kinachojiendesha chenyewe (Automatic Weather Station) katika Wilaya yake na kuahidi kuwa uongozi wa wilaya ya Lushoto utahakikisha matokeo ya utafiti yanakuwa endelevu Akizungumza kwa niaba wa wazee wa asili na wakulima wa Wilayani Lushoto,Bw. Benard alisema kutokana na mabadiliko ya tabia nchi baadhi ya viashiria vinapotea hivyo kwa kushirikiana na utabiri wa kisayansi hii itasaidia wakulima kujua hali ya hewa sahihi na pia kuwepo kwa kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini kwa kushirikiana na SUA kupitia msimamizi wa mradi Profesa Henry Mahoo wamezindua rasmi huduma ya FarmSMS ambapo mkulima ataweza kupata utabiri wa hali ya hewa, ushauri na tahadhari za hali ya hewa kupitia simu ya mkononi.
Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt.Agnes Kijazi akifafanua jambo kwa wakulima na watabiri wa asili.
Baadhi ya wakulima na watabiri wa asili wakifuatilia uzinduzi wa FarmSMS.
Bw.Edwin Ligenge, mtaalam kutoka TMA akieleza jinsi ya kujiunga na huduma ya FarmSMS.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Bw. Charles Moshi(wa tano kutoka kulia mstari wa mbele), Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi( wan ne kutoka kulia mstari wa mbele), Msimamizi wa mradi na mwakilishi kutoka SUA Prot. Mahoo (wa pili kutoka kushto mstari wa mbele) katika picha ya pamoja na wataalam kutoka TMA, SUA na watabri wa asili na wakulima.


mapitio ya magazeti leo


Ujumbe wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania TMF watembelea ofisi za Changamoto

Afisa Uhakiki wa Miradi ya Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania(Tanzania Media Fund) TMF.Sanne Vanden Barg akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari wa magazeti ya Changamoto na The Football wakati ujumbe wa TMF ulipotembelea katika ofisi za Ladyband zilizopo mtaa wa Daima Mikocheni jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Miradi wa TMF Alex Kanyambo na Kushoto ni Naibu Mhariri Mtendaji wa Gazeti hilo Samson Kamalamo.


Washindi wapatikana mashindano ya ngoma za asili Mkoa wa Tabora

Mgeni rasmi katika mashindano ya ngoma za asili kwa Mkoa wa Tabora Mstahiki Meya wa manispaa ya Tabora Gulamhussein Remtullah akizungumza na wakazi wa Mkoa huo katika mashindano hayo chini ya udhamini wa kampuni ya Bia Tanzania kupitia bia yake ya Balimi Extra , mashindano hayo yamefanyika katika shule ya sekondari Iyungi.tolle
Kushoto meneja wa matukio wa kampuni ya Bia Tanzania - tbl kanda ya ziwa Bwana Erick Mwayela akimkabidhi Meya wa Manispaa ya Tabora Mstahiki Meya Gulamhussein Remtullah kitita cha shilingi laki sita ikiwa ni zawadi ya mshindi wa kwanza wa mashindano ya Ngoma za asili kwa mkoa wa Tabora mashindano hayo yamedhaminiwa na kampuni ya Bia Tanzania kupitia Bia yake ya Balimi Extra kulia aliyevaa fulani ya balimi ni kiongozi wa kundi la Mwenge la manispaa hiyo ambao ndio wameibuka washindi wa shindano hilo.
Meya wa Manispaa ya Tabora katikati Akimkabidhi kiongozi wa kundi la Mwenge fedha tasilimu shilingi laki sita mara baada ya kundi hilo kutangazwa Washindi wa shindano la ngoma za asili kwa mkoa wa Tabora ambalo limefadhiriwa na kampuni ya Bia Tanzania Tbl kupitia Bia yake ya Balimi Extra kulia kwake ni Meneja matukio wa kampuni hiyo kanda ya Ziwa Bw Eric Mwayela.