Maofisa wa Polisi wanaoshughulikia Dawati Jinsia na Watoto Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wakifuatilia mafunzo yaliyoratibiwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) ambayo yamefanyika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo.
Mwezeshaji wa mafunzo ambaye ni Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, John Simtowe akitoa mada katika mafunzo hayo kwa maofisa wa Polisi wilayani humo ambayo yameratibiwa na TGNP.
Mafunzo yanaendelea kwa maofisa wa Polisi wanaoshughulikia Dawati Jinsia na Watoto Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwezeshaji, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, John Simtowe wakati akitoa mada.
Mkaguzi wa Polisi Dawati la Jinsia na Watoto Makao Makuu ambaye pia ni mwalimu wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia, Mohamed Mcheu akichangia katika mafunzo hayo kwa maofisa wa Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...