Taasisi
ya Global Education Link imeisaidia Serikali kuzalisha rasilimali watu wenye
ujuzi na elimu ya kutosha ili watumike katika kuinua viwanda na uchumi wa nchi.
Hayo
yamesemwa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo,
Abdulmaliki Mollel alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi
wa maonesho ya kwanza ya viwanda Tanzania yaliyofanyika katika viwanja vya Sabasaba
vilivyopo jijini humo.
Mollel
amesema kuwa Tanzania imeamua kuwa nchi ya viwanda lakini bila kuwa na
rasilimali watu wenye ujuzi na elimu ya kutosha kuhusu uzalishaji na
uendelezaji wa viwanda hakutakuwa na maendeleo kwani maendeleo yoyote mzizi wake
ni elimu na ujuzi.
“Kuna baadhi ya masomo ambayo ni muhimu hayapatikani
katika vyuo vya Tanzania na kama zinapatikana basi nafasi ni chache
hivyo,taasisi hii ni kama daraja la kutengeneza rasilimali watu wenye ubora
watakaoleta maendeleo ya nchi kupitia kusoma nchi za nje,”alisema Mollel.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...