Mwenyekiti
wa Kamati ya Harambee ya Kuwasaidia
waandishi wanaougua maradhi mbali mbali, Bw. Benjamin Thompson
akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani), ndani ya
Idara ya Habari MAELEZO,mapema leo jijini Dar kuhusiana na matokeo ya
harambee ya Media
Car Wash for Cancer Campaign, inayoendelea nchini.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Harambee ya Kuwasaidia
waandishi wanaougua maradhi mbali mbali, Bw. Benjamin Thompson
akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani), ndani ya
Idara ya Habari MAELEZO,mapema leo jijini Dar na pia akiwa ameambatana na baadhi ya
Waandishi wa habari watatu, Adolf Simon Kivamwo, Athumani Hamisi na Danstan Bahai (hayupo pichani) ambapo leo wamekabidhiwa jumla ya TZS 20m/- kwa ajili ya kulipia gharama za matibabu yao.
Waandishi wa habari watatu, Adolf Simon Kivamwo, Athumani Hamisi na Danstan Bahai (hayupo pichani) ambapo leo wamekabidhiwa jumla ya TZS 20m/- kwa ajili ya kulipia gharama za matibabu yao.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Harambee ya Kuwasaidia
waandishi wanaougua maradhi mbali mbali, Bw. Benjamin Thompson
akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh.Milioni 10 kwa Mwenyekiti
wa Chama cha Waandishi wa habari ZA Ukimwi (AJAAT), Adolf Simon Kivamwo kutokana na kusumbuliwa na Kansa ya Utumbo.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Harambee ya Kuwasaidia
waandishi wanaougua maradhi mbali mbali, Bw. Benjamin Thompson
akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh.Milioni Tano kwa aliyekuwa
mwandishi wa magazeti ya Habari leo na Daily News ambaye alipata ajali
na kumsababishia ulemamvu,Athman Khamis .
Waandishi wa habari watatu, Adolf Simon Kivamwo,
Athumani Hamisi na Danstan Bahai wamekabidhiwa jumla ya TZS 20m/- kwa ajili ya
kulipia gharama za matibabu yao.
Mwenyekiti wa Kamati ya Harambee ya Kuwasaidia
waandishi wanaougua maradhi mbali mbali, Bw. Benjamin Thompson alisema kuwa
fedha hizo ni matunda ya harambee ya Media
Car Wash for Cancer Campaign, inayoendelea nchini.
Kama tujuavyo, kwa kuanzia, wanahabari kutoka
vyombo mbalimbali Jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na wadau wengine
waliosha magari kwenye viwanja wa Leader Club Julai 4, 2015.
Alisema katika harambee hiyo jumla ya 31m/-,
zilipatikana, ambapo kati ya fedha hizo, ndizo wagonjwa wamegawiwa.
“Malengo yetu ya awali yalikuwa kwamba tuwachangishe
fedha kwa ajili ya wenzetu wagonjwa, pia kiasi kingine kitumike kuwaingiza
baadhi ya wanahabari kwenye mifuko rasmi ya Bima ya Afya. Na ndivyo
tulivyofanya leo hii,” alisema.
Bw Thompson alisema kiasi kilichosalia kitatumika
kuwaingiza waandishi wa habari 100 katika mpango wa kulipia matibabu kupitia mfuko
wa Bima ya Afya, yaani NHIF.” Alisema.
Alisema lengo la harambee hiyo ni kukusanya jumla
ya 100m/- kabla ya mwezi Disemba 2015 na kazi yake kubwa itakuwa kuwahudumia
wanahabari wasiojiweza kwa sababu ya kusumbuliwa na maradhi mbalimbali.
Pia pesa zitokanazo na harambee hiyo zitasaidia
kuanzisha mkakati wa mkubwa wa kuhakikisha wanahabari wote nchini wanaingizwa
kwenye mfuko wa Bima ya Afya.
“Lengo letu ni kuhakikisha wanabari wana kinga za
afya zao,ili tukomeshhe huu mtindo wa kuchangiana mara kwa mara kila mmoja
anapougua,”alisema na kuongeza kuwa watakaohusika katika zoezi hilo, ni wale wasioajiriwa
pamoja na wasioajiriwa lakini hawana huduma ya Bima ya Afya.
Ili kuendeleza mchakakato wa kufikia lengo kuu,
wanahabari Kanda ya Ziwa kwa kushirikiana na wenzao wa Jijini Dar es Salaam,
Agost 15 mwaka huu, wataosha magari kwenye viwanja vya Furahisha Jijini Mwanza.
Tunaomba wadau mbalimbali waungane nasi kwenye
hili,ikiwemo kulipia gharama mbalimbali ukiwemo usafiri kwenda na kurudi
Mwanza,hoteli, matangazo ya radio na mabango.
Wakati huo huo Bw Thompson amesema kutakuwa
mkutano wa wadau habari Jumamosi Agost 1, mwaka huu utakaofanyika Msimbazi
Centre Jijini Dar es Salaam kwa jili ya kuanzisha mchakato wa usajili wa rasmi
wa kampeni hii.
“Tunaomba wanahabari wote nchini watakaoweza
kuhudhuria wasikose kufika, maana hapa ndipo juhudi za ukombozi wa kiafya kwa
wanahabari zitakapoanzishwa rasmi,” alisema.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo alisema kuwa Kamati yake
imewashirikisha wahariri wote nchini katika kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa
na kwamba viongozi hao wa vyumba vya habari ndio waliotoa majina hayo kwa
kamati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...