Balozi
wa Tanzania Nchini Ubelgiji Dkt. Diodorus B. Kamala akielezea lengo la
ujio wa wawekezaji kutoka Ubelgiji kuja kuwekeza nchini Tanzania
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufuatia ujio wa wawekezaji
wa nchi hiyo Zanzibar. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar
Waziri
wa Miundombinu na Mawasilino Juma Duni Haji akiwa na watendaji wake
wakuu wakimsikiliza Meneja mauzo wa Kampuni ya ujenzi ya Anglo Belgian
Corporation ya Ubelgiji walipofanya mazungumzo Ofisini kwake Kisauni.
Wamiliki
wa makampuni toka Ubelgiji wakimsikiliza Mkurugenzi Uenezi wa Mamlaka
ya Uendelezaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) Bi. Nasria Mohd Nassor
(hayupo pichani) walipofika ofisini kwake Maruhubi Mjini Zanzibar.
Afisa
Mipango wa Shirika la Bandari Zanzibar Ali Haji akizungumza na
wamiliki wa makampuni kutoka Ubelgiji walipotembelea bandari ya Malindi
mjini Zanzibar .
Waziri
wa Fedha Omar Yussuf Mzee akizungumza na ujumbe wa Wafanyabiashara wa
Makamupuni ya uwekezaji kutoka Ubelgiji walipomtembelea Ofisini kwake
Vuga Mjini Zanzibar.
Picha ya pamoja ya wawekezaji kutoka nchini Ubelgiji na viongozi wa Mamlaka ya Uendelezaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA).(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
Mtaji wa $300,000 wamenusa hela za MCC phase 2? 700Bil
ReplyDeleteHawa wawekezaji tunawaleta wenyewe? Kwani gesi imegundulika na mafuta yako mbioni wawekezaji wa nini tena?