Mbu anayeambukiza kidinga popo

Nchini Tanzania watu 147 wamethibitika kuwambukizwa ugonjwa wa homa ya kidinga popo yaani homa ya dengu huku mtu mmoja akiripotiwa kufariki dunia kwa ugonjwa huo.
Kasi ya ugonjwa huo ambao ikiwa hautadhibitiwa unaweza kuleta madhara dalili zake zinashabihiana na zile za malaria kwani unaambukizwa kwa kupitia mbu na unadaiwa kusambaa katika maeneo mengine nchini Tanzania ingawa kwa sasa uko zaidi mjini Dare salaam.
Taarifa zinasema kuwa kuna visa vya wagonjwa nchi jirani ya Msumbiji taifa linalopakana na mkoa wa Mtwara jambo linalozua wasiwasi wa kuwa na visa vingine mkoani humo. Kutaka kufahamu hatua zinazochukuliwa na serikali ya Tanzania Joseph Msami amezungumza na Dk Janet Mgamba ni kaimu mkurugenzi msaidizi wa udhibiti na ufuatailiaji wa magonjwa ya milipuko ambaye anaanza kwa kueleza hali ya kidinga popo ilivyo.

(SAUTI MAHOJIANO)
KUSIKILIZA BONYEZA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. kidinga popo ndio homa gani? naomba mtuwekee kwa kiingereza au lugha ya kitaaluma.

    ReplyDelete
  2. He! homa hii ni hatari sana, mimi jirani yangu ameipata, ila kwa kuwa alisafiri kwenda nchi za Asia ambamo homa hii ipo kwa wingi nikajua kaitoa huko, kumbe inawezekana kaambukizwa hapa hapa nchini, balaa.Magonjwa yanazidi kuongezeka, Mungu tuhurumie watanzania.

    ReplyDelete
  3. Nadhani hapa wengine tunahitaji jina la kitaaluma. ndio¨homa gani hii? Kama ugonjwa hatari unazuka nchi jirani nadhani solution ni kufunga mpaka na nchi husika, kuzuia muingiliano.

    ReplyDelete
  4. Ni Dengue Fever

    ReplyDelete
  5. someni mpaka chini msikurupuke tu.wavivu wa kusoma.

    ReplyDelete
  6. Kitaalam inaitwa DANGUE FEVER

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...