Wauzaji wa pembejeo ambao sio waaminifu wamepewa onyo kali na endapo atabainika yeyote anayewalaghai wakulima na kuwauzia pembejeo ambazo sio hali hatua kali dhidi yake zitachukuliwa.

Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida Beatus Chowaji ametoa onyo hilo wakati akizindua mradi wa Faida Mali unaoshirikiana na shirika la AMDT katika kuwasaidia wakulima wa alizeti Mkoani Singida ili kulima zao hilo kibiashara zaidi.

Chowaji amesema kumekuwepo na malalamiko kwa baadhi ya wakulima ambao hukumbana na wauzaji wa pembejeo ambao sio waaminifu na kuwalaghai kwakuwa wakulima hao hawana elimu na uelewa hasa wa viuatilifu au mbegu ambazo ni halisi.

Ameongeza kuwa mkono wa serikali ni merfu na utawabaini popote walipo hivyo waache mara moja kwani kwa kufanya hivyo wanakirudisha nyuma kilimo cha alizeti ambacho ni tegemeo kwa ajili ya uchumi wa viwanda Mkoani Singida.

“Singida tuna Viwanda vya kuamua mafuta ya alizeti vikubwa viwili, vya kati vitatu na vidogo 115 na kufanya jumla ya viwanda vya alizeti kuwa 120, vyote hivyo vinategemea alizeti ya mkulima, lakini pia mkulima anakuwa na matarajioa makubwa, hao wauzaji pembejeo wasio waaminifu hatutawavumilia, tena waache mara moja”, amesisitiza Chowaji.

Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida Beatus Chowaji akisoma bango mara baaa ya kuzindua mradi wa Faida Mali unaoshirikiana na shirika la AMDT katika kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida.

Mkurugenzi wa Shirika la AMDT Michael Kayombo akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa Faida Mali wenye lengo la kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida kulima kibiashara.

Baadhi ya wadau waliohudhuruia uzinduzi wa mradi wa Faida Mali wenye lengo la kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida kulima kibiashara.

Mkurugenzi wa mradi wa Faida Mali mkoa wa Singida Tom Silayo akisoma taarifa ya mradi huo kwa wajumbe waliohudhuria uzinduzi wa mradi utakaowasaidia wakulima kulima alizeti kibiashara.

Mtendaji Mkuu wa Chama cha wasindikaji wa Mbegu za alizeti Tanzania Daud Musa Mwasantaja akiwahakikishia wakulima wa alizeti upatikanaji wa soko katika uzinduzi wa Mradi wa Faida Mali.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...