Habari nyeti zimevuja sasa hivi kuwa Ngoma Africa band aka FFU UGHAIBUNI  bendi maarufu ya muziki wa dansi barani Ulaya yenye makao kule nchini Ujerumani inatua nchini Israel kutumbuiza katika onyesho maalum la siku ya uhuru wa nchi hiyo ijulikanayo kama  Yom Haatzmaut siku ya tarehe 1 mpaka 2 Mei 2017 mjini Tel Aviv.
Mmoja ya wanaitifaki wa maonyesho hayo Bi.Shimone amesema bendi hiyo ndio ya kwanza ya Kiafrika kupata mwaliko wa kutumbuiza katika maonyesho hayo lakini hakutaka kuelezea zaidi.
Habari zaidi za uhakika zimevuja kuwa bendi hiyo imesafiri kimya kimya kutoka Ujerumani kuelekeahuko Uyahudini kwa ajili ya onyesho  hilo. Kiongozi wa bendi hiyo Kamanda Ras Ebrahim Makunja amethibitisha mwaliko huo wa kihistoria na kuiambia Globu ya Jamii kwamba wao hivi sasa wako Tel Aviv wakingoja kumwaga lazi.
 Kiongozi wa The Ngoma Africa Band wana FFU UGHAIBUNI akiongoza gwaride kujiandaa na libeneke la Israel
 Nyomi ya The Ngoma Africa Band wana FFU UGHAIBUNI katika moja ya maonesho yao
Kikosi kazi cha The Ngoma Africa Band wana FFU UGHAIBUNI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...