Mwenyekiti wa Jumuiya ya watanzania wanaosoma Beijing Nchini Husein Mtoro ( katikati) aliyemwakilisha Balozi,aliambatana na Viongozi wote Wakuu akiwemo Makam Mwenyekiti Khamis Ngwali,Katibu Mkuu Ndugu Remidius Emmanuel,Naibu Katibu Mkuu Ndugu Alinanuswe Mwakiluma na Mweka Hazina Ndugu Kulwa Gamba.
 
Pamoja nao,Viongozi waasisi wa Umoja huo Ndugu Suleiman Serera na Irenius Kagashe nao walishiriki sambamba na Viongozi wastaafu wengine akiwemo Makam Mwenyekiti Mstaafu Ndugu Kassim Jape,Katibu Mkuu Mstaafu Angelina Makoye,Mtunza Hazina Mstaafu Lusekelo Gwassa katika maadhimisho ya muungano yaliyofanyika mapema wiki hii kwa kushriki maonesho ya utalii na utamaduni.
Baadhi ya watanzania wanaosoma katika chuo cha Beijing nchini China wakiwa katika maonesho ya utamaduni na utalii kama moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanzania mapema wiki hii.
Wadau wakipozi kwa picha
Maonesho ya utalii na utamaduni yakiendelea Jijini Beijing

Jumuiya ya Wanafunzi Watanzania wanaosoma nchini China,wameadhimisha kumbukumbu ya Miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kushiriki MAONYESHO YA KIMATAIFA YA UTALII NA UTAMADUNI katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Biashara na Uchumi jijini Beijing.
 

Akizungumza kwa niaba ya Balozi wa Tanzania nchini China Balozi MBELWA KAIRUKI,Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo,ndugu HUSSEIN MTORO aliwaasa Watanzania hao kudumisha Amani,Mshikamano na kushiriki katika ajenda muhimu za Taifa ikiwemo,kushiriki katika kukuza soko la Utalii kwa kutangaza Vivutio vya asili vya nchi yetu,kuhamasisha Watalii wengi wa kimataifa kutembelea vivutio mbali mbali vilivyopo Tanzania.Pia Mwenyekiti alifikisha salam za Balozi Mbelwa za kuwatakia kila la heri Wanafunzi wote walio katika hatua mbalimbali za kukamilisha Tafiti zao kwa ajili ya kukamilisha masomo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...