Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Chiku Galawa (aliesimama) akizungumza mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) pale kamati hiyo ilipofanya ziara ya kukagua miradi ya Umeme Songwe Vijijini, katika Kikao kilichofanyika leo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Songwe.
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Livingstone Lusinde akifafanua jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati hiyo, pale walipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wa Ileje tayari ya kwenda kukagua Mradi wa Umeme uliopo kijijini hapo, Kushoto wake ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Dkt. Medard Kalemani na Kulia kwake ni Katibu Kamati wa Bunge anaehusika na Hesabu za Serikali (PAC) Ndg. Asmin Kihemba na anaefuata ni Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mhe. Joseph M. Mkude. katika kikao kilichofanyika leo katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wa Ileje Mkoani Songwe.
Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mhe. Joseph M. Mkude (aliesimama) akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) pale kamati hiyo ilipomtembelea Ofisi kwake tayari kwa Ukaguzi wa mradi wa umeme katika moja ya kijiji kilichopo Wilaya ya Ileje, Katika kikao kilichofanyika leo katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) walipotembelea na Kukagua Mradi wa Umeme uliopo moja ya kijiji kilichopo Wilaya ya Ileje Mkoani Songwe.(PICHA NA OFISI YA BUNGE).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...