Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili ( MNH), Profesa Lawrence Museru leo amekutana na wahudumu wa Afya katika hospitali hiyo pamoja na mambo mengine amewasisitiza kufanya kazi kwa bidii na kwamba uongozi wa hospitali hiyo utaendelea kutatua changamoto zinazowakabili.
Pia, mkurugenzi huyo amewataka wahudumu hao kuzingatia maadili ya kazi ili kutoa huduma bora kwa wagonjwa.Profesa Museru ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam katika mkutano na baadhi ya wahudumu wa afya uliolenga kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo.
Profesa Museru amesema licha ya wahudumu hao kukabiliwa changamoto mbalimbali , lakini hawanabudi kufanya kazi kwa bidii kwani jukumu lao ni kutoa huduma bora.
" Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayofanya hatua ambayo imesaidia kupunguza malalamiko wakati wa kutoa huduma , ingawa bado kuna changamoto lakini hatua budi kutoa huduma bora na sisi tutaendelea kutatua changamoto hizo kadiri inavyowezekana ili kuhakikisha mazingira yetu ya kazi yanakua bora," amesema Profesa Museru.
Katika mkutano huo wahudumu hao wamewasilisha ajenda 14 ikiwamo ombi la kupatiwa mafunzo ili kuongeza ufanisi na kuboresha utendaji kazi wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akifafanua jambo kwenye mkutano huo. Kulia ni Mkurugenzi wa Uuguzi, Agnes Mtawa wa hospitali hiyo.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...