Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza Bw.Aidan Eyakuze akishiriki katika kikao alipowasilisha juu ya Mapango wa Sauti za Wananchi unaotekelezwa na Taasisi hiyo, ambapo alisema kwa kiasi kikubwa mpango huo umesaidia kuinua maisha ya watanzania hasa kwenye maeneo ya Sekta ya Afya na Mawasiliano.Wakati wa Vikao vya Mkutano wa Nne wa Mpango wa Uendeshaji wa Serikali kwa Uwazi(OGP) Nchini Ufaransa, Kushoto ni Mshiriki wa Mkutano huo Bw. Badru Rajabu.
Wajumbe wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza Bw.Aidan Eyakuze alipokuwa akiwasilisha juu ya Mapango wa Sauti za Wananchi unaotekelezwa na Taasisi hiyo, Wakati wa Vikao vya Mkutano wa Nne wa Mpango wa Uendeshaji wa Serikali kwa Uwazi(OGP) Nchini Ufaransa
Wajumbe wa Mkutano huo kutoka Mataifa Mbalimbali wakichangia mada mara baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza Bw.Aidan Eyakuze kuwasilisha taarifa juu ya Mapango wa Sauti za Wananchi ambao alieleza jinsi wanavyowasaidia wananchi kuwa na mchango katika utungaji wa Sera na kutathmini mipango ya serikali zao. PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO PARIS
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...