Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini NEC imebainisha
kwamba, ukosefu wa elimu ya kutosha kwa Wapiga Kura, ulisababisha mapungufu
mbalimbali kujitokeza katika uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 Mwaka jana.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo
Kailima Ramadhani (Pichani juu) aliyasema hayo jana Jijini Mwanza, katika Mkutano wa
tathmini kati ya NEC na Asasi za Kiraia kuhusu utoaji wa elimu ya Mpiga Kura
wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka jana.
Ramadhani alisema katika baadhi ya
Kata nchini, kulitokea mapungufu kadhaa katika zoezi la kupiga kura ikiwemo Kura
kuharibika kutokana na wapiga kura kuchora michoro na alaza zisizostahili
katika karatasi ya kupigia kura huku baadhi yao wakiandika matusi katika
karatasi hizo.
Hata hivyo Kailima alitanabaisha
kwamba, zoezi la utoaji wa elimu kwa mpiga kura, lilishindwa kufanikiwa zaidi kutokana
na baadhi ya Asasi za kiraia nchini kutoa elimu kinyume na mwongozi wa NEC, ambapo
baadhi ya Asasi hizo zilikuwa zikitoa elimu ya mpiga kura kwa kuangazia zaidi
matakwa ya wafadhiri wake.
Edwin Soko ambae ni mmoja wa Wadau
kutoka Asasi zilizohudhuria katika Mkutano huo ambao umejumuisha Asasi
mbalimbali kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa, amesema kuwa katika Uchaguzi wa Mwaka
jana, Asasi nyingi hazikuweza kuyafikia maeneo mengi hususani vijijini kwa
ajili ya Kutoa elimu ya Mpiga kura, hii ikiwa ni kutokana na ukosefu wa fedha
ambapo wameishauri Serikali kuwa na utaratibu wa kutoa ruzuku kwa asasi hizo
ili kutoa elimu hiyo katika chaguzi zijazo.
Kando ya Tathmini hiyo, Suala la
Kuahirishwa kwa Uchaguzi Visiwani Zanzibar likajitokeza, ambapo Wanahabari
walitaka kujua sababu za Uchaguzi huo kuahirishwa, na hapo ndipo Mkurugenzi wa
Uchaguzi kutoka NEC akatumia tena fursa hiyo kufafanua kwamba Uchaguzi Visiwani
Zanzibar uliahirishwa na Tume ya Uchaguzi Visiwani humo ZEC kutokana na tume
hiyo kubaini kasoro kadhaa katika karatasi zake za wapiga kura, kasoro ambazo
hata hivyo hazikujitokeza katika karatasi zilizokuwa zikisimamiwa na Tume ya
Uchaguzi nchini NEC ikizingatiwa kwamba ZEC na NEC ni tume mbili tofauti
zisizoingiliana katika majukumu.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Kailima Ramadhani akifungua Mkutano wa tathmini kati ya NEC na Asasi za Kiraia kuhusu utoaji wa elimu ya Mpiga Kura wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka jana.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Kailima Ramadhani akizungumza na Wanahabari Jijini Mwanza nje ya Mkutano wa tathmini kati ya NEC na Asasi za Kiraia kuhusu utoaji wa elimu ya Mpiga Kura wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka jana. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...