Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza na Vijana wa
Tanzania walioshiriki mkutano wa tatu wa Vijana kutoka nchi za Bonde la Mto
Nile (hawapo pichani) uliofanyika nchini Misri kuanzia tarehe 6 – 14 Novemba
2015 ukiwa na lengo la kubadilishana uzoefu kutoka nchi washiriki. Kulia ni
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akipokea zawadi ya
ngao kutoka kwa Bibi. Dorice Assenga (katikati) kwa niaba ya Vijana kutoka
Tanzania walioshiriki mkutano wa tatu wa Vijana kutoka nchi za Bonde la Mto
Nile uliofanyika nchini Misri kuanzia tarehe 9 – 16 Novemba 2015 ukiwa na lengo
la kubadilishana uzoefu kutoka nchi washiriki. Kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo
ya Vijana Bw. James Kajugusi.
Baadhi ya vijana wa Tanzania walioshiriki mkutano wa tatu wa Vijana kutoka
nchi za Bonde la Mto Nile uliofanyika nchini Misri kuanzia tarehe 9 – 16
Novemba 2015.Kutoka kushoto ni Baraka Chedego, Paul Simango na Rwihula Daniel
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akiwa katika picha
ya pamoja na Vijana kutoka Tanzania walioshiriki mkutano wa tatu wa Vijana
kutoka nchi za Bonde la Mto Nile uliofanyika nchini Misri kuanzia tarehe 9 – 16
Novemba 2015 ukiwa na lengo la kubadilishana uzoefu kutoka nchi washiriki.
Picha
na Frank Shija,WHVUM.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...