Na
Lydia Churi-NEC
TUME ya Taifa ya Uchaguzi
imewataka wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini ambao ni wasimamizi wa Uchaguzi
kuhakikisha wanakagua vifaa wanavyopokea vinavyosambazwa hivi sasa kwa ajili ya
Uchaguzi ili kuondoa dosari zinazoweza kujitokeza wakati wa Uchaguzi Mkuu.
Mkurugenzi wa Ununuzi na
Ugavi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Eliudi Njaila ameyasema hayo leo
jijini Dar es salaam wakati wakiwaonyesha waandishi wa habari karatasi za mfano
za kupigia kura zilizopokelewa na NEC kwa ajili ya kuanza kusambazwa nchini
kote.
Njaila amesema karatasi hizo
za kupigia kura zitakapowafikia wakurugenzi wa Halmashuri wazikague na hasa kuangalia
nembo ya NEC kama ipo sahihi pia waangalie majina ya wagombea na vyama wanavyoviwakilisha
kama viko sahihi na vinakidhi mahitaji ya majimbo yao ya Uchaguzi.
Aidha aliongeza kuwa karatasi hizo za kura zitasambazwa
katika kata zote ambapo kila kata itapewa karatasi za mfano wa kupigia kura 200
na zitagawiwa kwa wagombea wa ngazi zote
ili wawaelimishe wanachama wao namna ya kupiga Kura na kuonyesha mgombea yupo
katika namba ipi kama ilivyoonyeshwa katika karatasi hizo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa
Ununuzi na Ugavi wa NEC, karatasi hizo za mfano wa kupigia Kura kwa ajili ya
wagombea wa Urais, Ubunge na Udiwani zitasambazwa kuanzia sasa na ifikakapo
Oktoba 7 zitakuwa zimeshafikishwa nchi nzima.
Tume imekuwa ikiendelea
kupokea vifaa mbalimbali kwaajili ya Uchaguzi Mkuu na Mara vinapowasili katika
ofisi za Tume vinasafirishwa na kupelekwa katika majimbo yote ya Uchaguzi
nchini. Hadi sasa vifaa vyote vimekwisha sambazwa isipokuwa karatasi halisi za
kupigia kura ambazo zitasambazwa siku chache kabla ya siku ya Uchaguzi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...