Na Dotto Mwaibale
BOHARI
ya Dawa (MSD) imezindua rasmi taarifa yake ya mwaka 2013/2014 (Annual
Report), ambayo ilizinduliwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Bodi ya
Wadhamini wa MSD, Profesa Idris Ali Mtulia.
Akizungumza
katika hafla ya uzinduzi wa taarifa hiyo, Profesa Mtulia alisema
kupanda kwa huduma za usambazaji dawa, upatikanaji wa dawa kutoka
asilimia 55 hadi 85 ni jambo la kujivunia.
Kaimu
Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani alisema mpango wa MSD kwa sasa ni
kuanzisha maduka ya dawa ambayo yataendeshwa na MSD ambapo kwa kuanzia
hivi karibuni litazinduliwa mkoani Mbeya na baadae itafuatia mikoa Kanda
za Dar es Salaam, Mwanza na Moshi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa MSD, Profesa Idris Ali Mtulia (kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa taarifa ya MSD ya mwaka 2013/2014 uliofanyika Ofisi za MSD Keko jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa MSD, Profesa Idris Ali Mtulia (kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa taarifa ya MSD ya mwaka 2013/2014 uliofanyika Ofisi za MSD Keko jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani.
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa MSD, Johnson Mwakalitolo, akizungumza katika uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Profesa Idris Ali Mtulia, akizungumza katika uzinduzi huo.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...