Na  Bashir  Yakub.

Rufaa  ni  hatua  ya   kisheria  ambayo  hufikiwa  na  mhusika  katika  shauri  fulani  iwapo  hakurushishwa  na  maamuzi. Rufaa  sio  mpaka  uwe  umeshindwa  kabisa,  hapana. Yawezekana  ukawa  umeshinda  kesi  lakini  hukuridhishwa  na kiwango   ulichoshinda.Kwa  mfano  uliomba  wavamizi  waondoke  katika  nyumba yako   na  hapohapo  wakulipe  fidia. Mahakama  ikatoa  hukumu  kuwa  umeshinda  wavamizi  waondoke  katika  nyumba  yako  lakini  ikasema wasikulipe  fidia.

Mazingira  kama  haya  unakuwa  umeshinda  lakini  ukitaka  unaweza  kukata  rufaa  kulalamikia kutolipwa  fidia.  Kwa hoja  hii  tunaona  kuwa kumbe  kukata  rufaa  si  lazima  uwe  umeshindwa  badala  yake unaweza  kuwa umeshinda  lakini  ukawa  hukuridhishwa  na  vitu  fulani  katika  hukumu  ambavyo  unaweza  kuvikatia  rufaa  ili  navyo  uvipate. 

1.AINA  ZA  RUFAA  KATIKA  MASHAURI  YA  ARDHI.

Kisheria  rufaa  hutofautiana  kutokana   na  aina  ya  mgogoro  ulio  mbele. Mgogoro  wa  kimkataba  unazo  namna  zake   na  masharti yake  katika  rufaa, halikadhalika  migogoro  ya  kudai  fidia, migogoro  ya  kikazi, migogoro ya  kifamilia  na  talaka, migogoro  ya  jinai,  migogoro  ya  kibiashara n.k.  Hii  ina  maana  hata  migogoro  ya  ardhi  nayo  inazo  namna  zake  za  rufaa. Katika  mashauri  ya  ardhi   mara  nyingi  migogoro huanzia  baraza  la  ardhi  la  kata huenda  mabaraza  ya  ardhi  ya  wilaya, mahakama  kuu  ya  ardhi   hadi  mahakama  ya  rufaa.  

Hizi  zote ni  mamlaka  zinazoweza  kuamua  mashauri  ya ardhi.  Aidha  aina  za  rufaa  huweza  kutokana  na  mpangilio huu  kimahakama. Ipo  rufaa  inayotoka  baraza  la ardhi  la  kata  kwenda  baraza  la  ardhi la wilaya. Ipo  rufaa  kutoka  baraza  la  ardhi  la  wilaya  mpaka  mahakama  kuu  ya  ardhi. Na  ipo  itokayo  mahakama  kuu  ya  ardhi  mpaka mahakama  ya  rufaa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...