Mwenezi
wa CCM Mkoa wa Dar Es Salaam Ndugu Juma Hamis 'Gadafi' akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye hotel ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakielezwa na Mwenezi wa CCM Mkoa wa Dar Es Salaam Ndugu Juma Hamis 'Gadafi' alipozungumza nao mapema leo mchana kwenye hotel ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakielezwa na Mwenezi wa CCM Mkoa wa Dar Es Salaam Ndugu Juma Hamis 'Gadafi' alipozungumza nao mapema leo mchana kwenye hotel ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Chama Cha Mapinduzi
mkoa wa Dar es Salaam kimeitaka
Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuongeza,vifaa na rasilimali watu ili wananchi wengi
waweze kujiandikisha kwenye Daftari la kudumu la wapiga kura bila usumbufu.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu
wa Siasa na Uenezi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Bw. Juma Simba Gadafi alisema anawashukuru waandishi kwa
ushirikiano waliounesha kwenye mkutano
wa kumtambulisha mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli
uliofanyika tarehe 14 Julai 2015 katika viwanja vya Mbagala Zakheem.
Aidha aliwataka wakazi wa jiji la Dar es Salaam kujitokeza
kwa wingi siku ya tarehe 1 Agosti 2015, kupiga kura za maoni kuchagua wagombea Udiwani
na Ubunge .Katika mkutano huo ambao waandishi wengi walionekana kuwa na
shauku ya kutaka kujua maoni ya CCM juu ya kuondoka kwa Edward Lowassa , Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam alisema “Lowasa
aliingia mwenyewe CCM bila shinikizo na kutoka mwenyewe hivyo maamuzi yake hayaifanyi
CCM ishindwe kuendelea kutekeleza majukumu yake”.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...