Na FG BLOG.
Wanahabari wa mkoa wa Iringa
leo wamekutana na kamanda wa polisi na maofisa wa jeshi la polisi Mkoani
hapa ili kuendelea kufanya Kazi kwa ushirikiano kwa faida ya Mkoa wa
Iringa.
Katika kikao hicho kilichoambatana na semina fupi ya kukumbushana wajibu wa Kazi za wanahabari na askari.
Akitoa
mafunzo hayo kamanda wa polisi wa Mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi amesema
kuwa ili kuufanya Mkoa wa Iringa uweze kufanikiwa ni lazima wabahabari
na polisi kufanya Kazi zao kwa kuzingatia maadili na kutofanya upendeleo
katika utendaji wao.
Mungi
alisema kuwa mbali ya kazi kubwa ambazo vyombo vya habari mkoani hapa
vinafanywa bado jeshi lake limeamua kukutana na wanahabari hao ili
kizidi kuufanya Mkoa kuwa na taswira nzuri ktk mahusiano Kati ya pande
hizo mbili kama njia ya kuwatumikia wananchi.
Alisema
kwa Mkoa wa Iringa vyombo vya habari vimeonyesha mchango mkubwa zaidi
zaidi na kutaka mchango huo na jitihada hizo kuendelea zaidi .
Kamanda
Mungi amesema kuna haja ya wanahabari na askari polisi kuendelea
kujenga mahusiano kwa kukutana na viongozi wao kabla ya kufanya
mapambano yasiyo na tija.
Alisema
kuwa wao kama jeshi la polisi wanatambua kuwa vyombo vya habari ni
muhimu kwa jamii hivyo lazima kujenga mahusiano mema na kuwa askari
polisi hawanasababu ya kuendeleza mivutano
Alisema
kuwa kuna wakati mwingine ajali imetokea na Kazi ya mwanahabari ni
kuhabarisha umma na polisi kuokoa hivyo lazima kufanya Kazi kwa karibu
na kutoa majibu stahiki kwa wanahabari na wanahabari kutotumia jazba
katika utendaji Kazi zao .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...