Dar es Salaam, Jumanne, Machi 3, 2015 – Serikali ya Tanzania itatoa taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa! (BRN), Alhamisi; tarehe 5 Machi 2015, kuhusu utekelezaji wa mikakati iliyowekwa katika Sekta Sita za Kipaumbele (NKRAs) zilizotekelezwa katika mwaka 2013/14. Sekta hizo ni: Kilimo, Elimu, Nishati, Uchukuzi, Maji, na Utafutaji Raslimali Fedha.

Ripoti ya Mwaka ya BRN imeandaliwa kuendana na utamaduni wa BRN wa kuweka vipaumbele, malengo na mfumo wa utekelezaji unaoendana na uwekaji wa mikakati ya kina ya kusimamia ufuatiliaji; pamoja na utumishi makini wa wafanyakazi wanaosimamia na kutekeleza kwa uwazi.

Umma unaalikwa katika maonesho ya miradi ya BRN yatakayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City kuanzia saa saba mchna hadi saa 11 jioni ili kupata fursa ya kuufahamu zaidi mfumo huu na mikakati inayoendelea kutekelezwa.

Katika tukio hilo wananchi pia watapata fursa ya kukutana na watekelezaji pamoja na walengwa wa miradi ya BRN, ambao watazungumzia uzoefu wao kuhusu safari ya mabadiliko wanayoiona na jinsi mabadiliko ya kiutendaji yaliyoletwa na BRN yanavyoboresha maisha yao.

Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...