Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Kilwa Road jijini Dar es Salaam, Lucas
Mgaya(wa pili kushoto) akimkabidhi kikombe mchoma nyama mkuu wa
Bar Chamanzi, Shaban Seif mara baada ya kuibuka mabingwa katika
mashindano ya Safari Nyama Choma kitongoji cha Dar One Temeke Dar
es Salaam yaliyofanyika katika Uwanja TCC Chang’ombe mwishoni mwa
wiki.Kushoto ni Meneja wa bia ya Safari Lger, Edith Bebwa.
Na Mwandishi Wetu.
KILWA ROAD Bar Dar One Temeke jijini Dar es Saalaam wameibuka mabingwa
katika fainali za mashindano ya Safari Lager Nyama Choma 2015 yaliyofanyiaka
mwishoni mwa wiki katika viwanja vya TCC Chang’ombe na hivyo kuzawadiwa
Kikombe pamoja na nafasi ya kushiriki fainali za Mkoa zinazotarajiwa kufanyika
Aprili 12,2015 katika viwanja vya Leaders.
Nafasi ya pili ilichukuliwa Liquid Bar ambayo kwa nafasi hiyo ilipata nafasi ya
kushiriki fainali za Mkoa Leader na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Chamanzi Bar
ambao pia walipata nafasi ya kushiriki fainali za Mkoa pale Leaders.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...