Na Bashir Yakub.

Kipindi cha nyuma wakati nikieleza masuala ya sheria za ndoa niliwahi kueleza utaratibu wa mgawanyo wa mali iwapo ndoa inavunjika. Kimsingi nilieleza mgawanyo wa mali katika msingi wa uwepo wa ndoa ya mke mmoja. Sikuwahi kueleza mgawanyo wa mali iwapo ndoa ni ya mke zaidi ya mmoja. Wengi waliuliza swali hili ambapo baadhi niliwajibu na baadhi sikuwajibu. Leo sasa nitaeleza mgawanyo wa mali katika ndoa ya mke zaidi ya mmoja pale ambapo mmoja wa wake inatalakiwa .

1.NDOA YA MKE ZAIDI YA MMOJA.

Kwa jina la kitaalam ndoa za namna hii huitwa ndoa za mitala. Waolewaji waweza kuwa wawili, watatu , wanne, watano au zaidi neno mitala hubaki kuwa mitala. Sheria yetu ya ndoa inatambua ndoa ya mke zaidi ya mmoja na hivyo kwa waliofanya hivyo hawajatenda dhambi yoyote kisheria. Ndoa za namna hii mara nyingi zimekuwa zikifungwa na waislamu au watu ambao huishi maisha ya kufuata mila ambao wengi wao wako vijijini. Hata hivyo tumeshuhudia mazingira ya ndoa za namna hii kwa watu ambao ni wa makundi tofauti na niliyotaja kwa siku za hivi karibuni. Yote kwa yote hizo ndio ndoa za mitala.

2.ISEMAVYO SHERIA YA NDOA KUHUSU MKE ZAIDI YA MMOJA.

Kifungu cha 57 cha sheria ya ndoa kinaweka wazi kwa kusema kuwa, katika sheria yoyote ile mwanaume anapokuwa na wanawake wawili au zaidi wanawake hao wanatakiwa kuwa na haki sawa mbele ya macho ya sheria na si vinginevyo. Kawaida tumezoea kuna u bi mkubwa na u bi mdogo. Basi ieleweke kuwa hayo ni mambo ya kwetu lakini sheria haina u bi mkubwa wala u bi mdogo. Sheria inajua mke ni mke awe alianza kuolewa au ameolewa mwishoni. Wake wote wana haki sawa mbele ya mme wao na mbele ya sheria na huo ndio msimamo wa sheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...