Na   Bashir  Yakub 

1. KUTAPELIWA  KATIKA  UNUNUZI  WA  GARI.

Ununuzi wa magari sawa na biashara nyingine yoyote unahitaji umakini. Lakini ununuzi wa  gari unahitaji umakini mkubwa zaidi pengine kuliko  mali nyingine yoyote inayohamishika kwa sasa. Hii ni kutokana na kukua kwa biashara ya bidhaa hiyo kulikoleteleza kujipenyeza  kwa matapeli hasa mijini. Utapeli  wa magari ni mkubwa kuliko watu wanavyofikiria na idadi ya wanaotapeliwa kwa siku inaelekea kulingana na idadi ya magari yanayouzwa kwa siku. Si  rahisi kulijua hili kama hufuatilii mambo haya. Uzuri au ubaya, wanaofanya matukio haya ni walewale. Nafasi kubwa wanayotumia ni ulaghai wa kimkataba na wanatumia mapungufu ya mkataba kumtapeli mtu halafu wanaendelea kuwapo na huna la kufanya sababu  mkataba wako una mapungufu ambayo uzito wake kisheria ni kama huna  mkataba. Aliyekutapeli atakuwapo na hutakuwa na la kufanya kwasababu ya msemo wa kisheria usemao “Buyer Be Aware”(Mnunuzi kuwa Makini). Umakini wako ni katika kufanya mkataba utakaolinda manunuzi yako. Lau ukifanya kosa  sheria imeshasema hivyo imemaliza. 

2. MKATABA SALAMA WA KUNUNULIA GARI  LAKO HAKIKISHA  UNA  TAARIFA   HIZI.

( a ) Lazima uwe na majina ya wahusika ambayo yatakuwa yameandikwa kwa urefu  na kwa kueleweka.Mfano jina liwe Aloys Mayenge Archard. Epuka kuandika vifupi  mfano A.M. Archard. Jina linatakiwa liwe katika ukamilifu wake na hasa pawe na majina matatu kamili. Pia majina  ya pande zote mbili yaani muuzaji na mnunuzi yatokee hivyohiyvo  si tu majina ya upande mmoja. Yawezekana mkataba mwingine unahusisha watu wengi zaidi  pia ni muhimu  majina matatu ya kila mmoja yaonekane hata kama  wako ishirini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...