·
Viingilio
shilingi elfu 15 kwenye vituo na elfu 20 mlangoni
Tamasha
la miaka kumi ya THT litakalofanyika jumamosi hii katika viwanja vya Escape 1
Mikocheni, limekamilisha maandalizi yake na hivyo kuwataka wadau na wapenzi
wake wajitokeze kwa wingi kushuhudia burudani kubwa ya mziki hapa nchini.
THT, ambayo
inasifika kwa kuzalisha wasanii mahiri nchini kama Linah, Barnaba, Mwasiti,
Ditto, Mataluma, Vumi, Beka, Recho, Marlaw, Msami, Makomando na wengine wengi,
imejipanga kutoa burudani kubwa ya mziki kwa mashabiki wake.
Akizungumza
kuhusu maandalizi hayo, Meneja Mkuu wa THT, Mwita Mwaikenda alisema maandalizi
yanaenda vema na mashabiki wahudhurie kwa wingi kujionea namna kituo hicho kilivyoweza
kufanya mapinduzi kwenye tasnia ya muziki.
‘Mpaka
sasa wasanii wa THT watakaotoa burudani wako tayari, na kama mnavyojua THT
utamaduni wake ni kupiga muziki kwa kutumia bendi lakini pia wasanii
watakaotusindikiza ni kama Ben Paul, Mrisho Mpoto na Weusi’ alisema Mwita.
Akizungumzia
wadhamini waliojitokeza kwenye shughuli hiyo, Mwita aliwashukuru Mr. Price
waliowavisha wasanii wote, Mziiki.Com ya Spice Afrika walionunua tiketi 500 za
tamasha kwa ajili ya wateja wao, SanMoto Pikipiki waliotoa pikipiki, Tanzania
Fashion and Design Limited, Darling Hair ambao wametoa nywele kwa waimbaji wote
wa kike na Clouds Media Group.
‘Tunatoa
shukrani za dhati kwa wadhamini wetu, kwa kutuunga mkono katika kuadhimisha
miaka kumi ya kuleta mapinduzi katika burudani’ alisema Mwita.
Tiketi za
tamasha zinapatikana maduka ya Robby One Fashion Kinondoni na Sinza, Yahya
Boutique Kinondoni, Born 2 Shine Mwenge, Ofisi za Clouds, Moca City Samora
Avenue, City Sports Lounge, Mr Price na THT Kinondoni.
Kiingilio
ni 15,000/- kwenye vituo hivyo na kwa wale wanaotaka za VIP ni 50,000/-
na zinapatikana THT pekee yake.
Siku ya
onesho pale Escape One, mlangoni kiingilio kitakuwa ni Shs 20,000/=.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...