Keki Maalum ambayo imeandaliwa na baadhi ya Wajumbe Wanawake wa Bunge Maalum la Katiba kumpongeza Mjumbe wa Bunge hilo Mh. Asha Bakari Makame kwa umahiri wake wa kupinga udhalilishaji wa kijinsia ndani ya Bunge hilo.
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Asha Bakari Makame akitoa shukrani zake kwenye hafla fupi ya Kupongezwa kutokana na kutetea jinsia ya Wanawake ndani ya Bunge la Katiba.
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Asha Bakari Makame akikata Keki Maalum kuashiria uzinduzi wa hafla fupi ya kupongezwa kwake kutokana na msimamo wake ndani ya Bunge Maalum la Katiba linaloendelea Mjini Dodoma.Kushoto yake ni Waziri wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Maendeleo ya Vijana wanawake na Watoto Mh. Zainab Omar Mohammed.
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Asha Bakari akimlisha Keki Mjumbe mwenzake wa Bunge hilo Mh. Zainab Omar Mohammed kwenye hafla fupi ya kupongezwa kwake.
Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Waride Bakari Jabu akitoa neno la shukrani kwenye hafla fupi ya Kupongezwa Mjumbe mwenzake Mh. Asha Bakari Makame kwa msimamo wake ndani ya Bunge hilo.
Hivi ndivo pesa za walipa kodi zinavotumika, WALLAHI Mola anawaona na ndio maana mwisho wenu unakuwa mbaya! sipati picha hawa ngulume ameishiaje!
ReplyDelete