Kikundi mahiri cha KAPOTIVE Star Singers- Bukoba,Wanayo furaha kuwatangazia kuwa kwa mapenzi ya Mungu, Tar. 20/04/2014 sikukuu ya Pasaka watakuwa na tamasha la Pasaka LINA’S CLUB -Bukoba, kuanzia saa 9 mchana hadi 2 usiku na kesho yake tar. 21/04/2014 Watakuwa katika mji wa Biharamulo. 

 Mratibu wa Tamasha hilo Bw. Andrew Kagya amesema kuwa Mwimbaji mgeni (Guest singer) atakuwa Flora Mbasha na kundi lake zima kutoka jijini Dar es Salaam na pia Kutakuwepo kwaya mbalimbali za RC, KKKT na SDA za hapa Bukoba.Kiingilio kitakuwa kama ifuatavyo:Mtu mmoja 10,000/-
Watu watatu  25,000/-,  Watoto 5,000/-
Kutokana na udhamini wa kinywaji maridadi cha Climax Non-Alcoholic Herbal drink, kila atakayenunua ticket ya 10,000, atapewa kinywaji kimoja cha Climax mlangoni, na atakayenunua ticket ya 25,000 atapewa CD moja mpya ya KAPOTIVE Star Singers (Zawadi ya Pasaka) na vinywaji vitatu vya Climax bure. Karibuni tusherekee ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristu kwa nyimbo na shangwe.Baadhi ya waimbaji wa Kapotive Star wakiimba kwenye matamasha yao yaliyopitaKazaliwa!! Njoo mumuone!!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Afican beauty jive or.......

    ReplyDelete
  2. Tuige mfano wa mavazi ya mama wa bwana wetu yesu.

    ReplyDelete
  3. ni muislam lakini naunga mkono mdau namba 2

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...